• TANZAKILIMO TANZANIA

    Pata taarifa sahihi kuhusu kilimo na ufugaji,kwa weledi wa hali ya juu

  • WATAALA WA KILIMO NA UFUGAJI

    Tunakupatia ushauri wa kitaalam katika maswala yote ya kilimo na ufugaji,toka kwa wataalam wetu waliobobea kwenye nyanja nzima ya kilimo. Wasiliana nasi kwa simu namba +255 675 117 151.

  • UNATAFUTA MASOKO YA MAZAO YAKO? UNATAFUTA MAZAO YA KUNUNUA?

    Tanzakilimo inakuunganisha na wakulima/wanunuzi na wadau wote wa maswala ya kilimo. Wasiliana nasi leo tukuunganishe na wadau....

Jumamosi, 27 Mei 2017

Black Australorp ( Kuku Weusi wa Malawi)


Australorp wanastahimili mazingira tofauti, kama kuku wa kienyeji aliye zoeleka nchini Tanzania. Na ni wazuri kwa ufugaji huria, kwa kuwaachia nje wajitafutie chakula wenyewe. Ingawa wanajulikana kwa sifa yao ya utagaji mayai mengi, lakini kuku hawa wanafaa kwa nyama pia, kwani huwa na nyama nyingi sana (dual purpose chickens)

Kuku hawa huweza kumpatia mfugaji faida kubwa, kwani ni wazuri kwa biashara ya mayai na nyama pia. Hawana sifa nzuri ya kulalia mayai, lakini akilalia hutotoa vifaranga vingi, na ni wazuri kwa uleaji wa vifaranga hivyo.

Utagaji wao wa mayai unakaribia ule wa kuku wa kizungu. Kuku hawa ni wakubwa, wazito, na wanamvuto sana kuwaangalia. Wanapendeza pia kwa ufugaji mdogo, katika mazingira ya nyumbani. Wana michirizi ya kijani pale wanapomulikwa kwenye mwanga mkali wa jua.

Kwa wastani Black Australorp, hufikisha mayai 250 kwa mwaka, wakiwa katika mazimgira mazuri. Kuku hawa ni wapole na rafiki kwa binadamu. Black Australorp ni wagumu, hawapati magonjwa mara kwa mara, hivyo basi huvumilia magonjwa ya aina nyingi, na hawachagui chakula. Wanakula vyakula wanavyo kula kuku wengine wa kienyeji. Huanza kutaga wakiwa na umri wa miezi mitano na nusu hadi sita.

Jogoo hufikisha kilo 3.5 – 5.0 na
Temba/hen hufikisha kilo 3.0 – 3.7

kwa mahitaji ya aina hii ya kuku,wasiliana nami kwa simu namba o716 71729o,tuko kigamboni,dar es salaam

Jumatano, 24 Mei 2017

LISHE YA KUKU NA KUCHANGANYA CHAKULA


LISHE YA KUKU:

Ili kuku waweze kuishi, kukua vizuri, kunenepa na kutaga mayai mengi ni lazima wale chakula kingi na chenye ubora unaotakiwa. Uwingi na ubora wa lishe ya kuku unaweza kuainishwa katika makundi ya vyakula kama ifuatavyo:

  1. Vyakula vya kutia nguvu

  2. Vyakula vya kujenga mwili

  3. Vyakula vya kuimarisha mifupa

  4. Vyakula vya kulinda mwili

  5. Maji.


MAKUNDI YA VYAKULA:





    1. Vyakula vya kutia nguvu:




Vyakula vya mifugo vifuatavyo vinawekwa katika kundi hili;

  1. Pumba za mahindi, pumba laini za mpunga, na, pumba laini za ngano.

  2. Nafaka kama vile mtama , chenga za mahindi ,chenga za mchele, uwele , na ulezi

  3. Mimea ya mizizi kama vile muhogo, viazi vitamu na magimbi. Kabla ya kulisha kuku hakikisha mizizi hiyo inalowekwa kwa muda wa saa moja au kupikwa kabla ya kukausha ili kuondoa sumu ambayo kwa asili imo katika vyakula vya aina hii.Inashauriwa kuwamizizi hiyo ilishwe kwa kiasi cha asilimia 10% ya chakula chote anacholishwa kuku.


Katika kundi hili la kutia nguvu ,vyakula vya mafuta kama vile mafuta ya kutoka kwenye vyakula vya mafuta kama mashudu ya mimea ya mafuta, mafuta ya samaki husaidia kuongeza nguvu na joto mwilini. Vyakula vya kutia nishati huchangia asilimia 60-70 ya mchanganyiko wote wa chakula.

  1. Vyakula vya kujenga mwili:


Ø  Mashudu :Haya ni makapi ya mbegu za mimea aina ya mikunde na vyakula v vinavyotoa mafuta kama vile alizeti, mawese, karanga, soya ,korosho, na ufuta .

Ø  Damu ya wanyama iliyokaushwa (waliochinjwa na kukaguliwa), hii inafanywa ili kuepusha uwezekano wa kuku kupata magonjwa ya kuambukiza .

Ø  Mabaki ya samaki ya samaki/dagaa na nyama.

Ø  Vyakula asilia kama vile minyoo, mayai ya mchwa, Masalia ya nyama toka kwenye ngozi/mifupa, wadudu walioteshwa kutokana na damu au nyama iliyooza na vyakula vya aina nyingine.

Ø  Vyakula hivi huchangia asilimia 20 hadi 30% ya mchanganyiko wote wa chakula cha kuku.

  1. Vyakula vya kuimarisha mifupa(madini): a)Hivi ni vyakula vya madini ambavyo huhitajika kwa ajili ya kujenga mifupa, maganda ya mayai, kukua na kuuweka mwili wa ndege (kuku) katika hali ya afya njema kwa ujumla.

  2. b) Madini ya muhimu ni madini ya chokaa (calcium) na fosiforasi (phosphorus). Ili kuku watage mayai yenye ganda gumu ni lazima wapate madini ya chokaa maganda ya konokono na mayai yaliyosagwa vizuri. Lakini inapendekezwa kwamba unapoongeza madini ya fosforasi inakubidi uongeze pia madini ya chokaa kadri inavyopasa ,kwasababu kiwango cha aina moja kikizidi kuliko cha aina nyingine husababisha upungufu wa kile kidogo


Viinilishe vya madini vinavyotakiwa ni pamoja na;

Ø  Majivu ya mifupa yaliyosagwa vizuri, unga uliosagwa wa magamba ya konokono wa baharini, konokono wa nchi kavu na maganda ya mayai yaliyochomwa . Kabla maganda ya mayai na nyumba za konokono havijatumika inashauriwa yachomwe moto mkali au yachemshwe ili kuua vijidudu vya maradhi.

Ø  Chumvi ya jikoni

Ø  Madini yaliyotengenezwa viwandani kama vile Di-calcium phosphate

Ø  Magadi (kilambo).

  1.     Vyakula vya kulinda mwili:


Kundi hili linajumuisha vyakula vya mbogamboga kama vile;

Ø  Mchicha, samadi ya ng’ombe ambayo haijakaa muda mrefu baada ya kunyewa, mchicha pori, Chinese kabeji n.k.

Ø  na Mchanganyiko wa vitamini uliotengenezwa na viwanda vya madawa (vitamin premix).

Ø  Jua ni muhimu katika kuhakikisha vitamini A na D zinatumika vizuri mwilini, kwahiyo banda ni lazima lijengwe kwa mtindo ambao unaruhusu mwanga kupita hasa nyakati za asubuhi na jioni.

Ø  Chakula cha kuku wanaofugwa ndani ni lazima kichanganywe na vitamini zinazotayarishwa viwandani.

          KUCHANGANYA CHAKULA CHA KUKU:


Njia za kuchanganya chakula cha kuku;

Kuna njia kuu mbili za kuchanganya chakula cha kuku, nazo ni;

Ø  Kuchanganya chakula kwa mashine;

o   Njia hii hutumika viwandani kuchanganya chakula kwa ajili ya kuku wanaofugwa katika mashamba makubwa.

Ø  Kuchanganya chakula majumbani (home made ration): Hii ni njia inayotumika kuchanganya chakula kwa ajili ya kulisha kundi dogo la kuku na njia ambayo inaweza kutumiwa na wafugaji wadogowadogo.

VIFAA; Beleshi /koleo(spade), Turubai/sakafu safi, Viinilishe , Viroba/Magunia kwa ajili ya kuhifadhia chakula kilichochanganywa.

Chakula kilichochanganywa kinaweza kuwekwa katika uzani wa kilo 25-kilo 50, au kilo 100.

                MCHANGANUO WA VIINILISHE VYA CHAKULA CHA KUKU:

 

Aina ya chakula                                   kiasi

  1. Vyakula vya kutia nguvu mwilini:


Ø  Pumba za mahindi            kilo   48

Ø  Pumba laini za mpunga    kilo   26

            Jumla                                            kilo 74

  1.      Vyakula cha kujenga mwili : 


                                       

    MASHUDU YA ALIZETI                                   KILO 18


Damu ya wanyama                                                                    kilo   1

Mabaki ya samaki /dagaa                                                          kilo   3

          JUMLA                                              KILO  22


iii.Vyakula vya kuimarisha mifupa (Madini):

  1. chumvi ya jikoni                                   kilo ½

  2. chokaa(dicalciumphosphate)…            kilo 2

  3. poultry premix/                                     kilo ½

  4.  unga wa mifupa                                  kilo 1


          Jumla                                                      kilo 4

  

Ø  Mahitaji halisi ya viinilishe kwa muhtasari:

Ø  Vyakula kutia nguvu mwilini                             kilo 74

Ø  Vyakula vya kujenga mwili                              kilo 22

Ø  Vyakula vya kuimarisha mifupa (Madini)        kilo 4

  JUMLA                                                                        100

Jumla ya mchanganyiko wa vyakula                kilo 100 

 


HATUA ZA KUCHANGANYA CHAKULA CHA KUKU:


HATUA YA KWANZA:

Katika hatua ya kwanza utaanza kuchanganya vyakula vya madini

Changanya , chokaa, chumvi na majivu ya mifupa pig mix vizuri - huu utauita mchanganyo Na.1

HATUA YA PILI:

Changanya mchanganyo huo na damu pamoja na samaki waliosagwa - huu utauita mchanganyo Na. 2

HATUA YA TATU:

Mchanganyo Na.2 uchanganye na mashudu vizuri ambao utauita mchanganyo Na.3.

HATUA YA NNE:

Mchanganyo Na.3 umwage juu ya rundo la pumba iliyochanganywa (pumba ya mahindi na pumba laini ya mpunga).

o   Chukua beleshi /koleo safi lililo kavu na kulitumia kuchanganya rundo la chakula ili kusambaza viinilishe vizuri.

Mambo ya kuzingatia katika kulisha na kutunza chakula cha kuku:

  1. a) Baada ya kuchanganya chakula kitawekwa kwenye viroba au magunia na kutunzwa ghalani (stoo) hadi pale kitakapohitajika kwa ajili ya kulisha kuku.

  2. b) Hakikisha kuku wanapata lishe kadri inavyopendekezwa na wataalamu.

  3. c) Chakula kilichochanganywa ni lazima kiwekwe sehemu kavu ili kisiharibiwe na unyevunyevu kama vile kwenye chaga mabanzi yaliyotandazwa juu ya mawe yalipangwa vizuri

  4. d) Chakula kilichoharibika hakifai kulisha kuku kwani kinaweza kusababisha matatizo ya afya.

  5. d) Chakula kilichochanganywa kinatakiwa kisikae muda mrefu baada ya kutayarishwa.


Vyakula vya ziada:

Ili kuhakikisha kwamba kuku wanapata viinilishe vya kutosha kuku wanaweza kupewa mchwa na mafunza.

Vilevile vitu mbadala aina ya nafaka vinavyopatikana hutegemea sana aina ya mazao yanayolimwa katika eneo husika.

Mbinu za kuotesha mchwa na funza: Funza na mchwa ni chakula kizuri na rahisi chenye viinilishe aina ya protini kwa kuku wanaofugwa kwa mfumo huria unaoboreshwa. Hata hivyo vyanzo hivi vya chakula cha protini huchangia tu vile ambavyo kuku wanatakiwa kupewa.

  1. Inashauriwa uwape vifaranga hao funza na mchwa kwa sababu ndio wanaohitaji protini kwa kiasi kikubwa na cha kuaminika.


Funza na mabuu yanaweza kuoteshwa kwa njia rahisi na kutumika kuboresha chakula cha vifaranga.

  1. c)Mafunza na mabuu yanaweza kuoteshwa kwa kutumia damu, viungo vya ndani ya tumbo la ng’ombe pamoja na samadi ya ng’ombe.

  2. d) Chungu kijazwe maji theluthi moja ya ujazo wake, inzi watakuja na kutaga mayai katika mchanganyiko ambao mafunza walioteshwa wataanza kula mchanganyiko huo.

  3. e) Baada ya hapo vitu hivi vyote vitachanganywa pamoja katika chungu kimoja kikubwa ambacho kitaachwa wazi wakati wa mchana na kufunikwa wakati wa usiku.

  4. f) Siku tano baadaye maji yatajazwa kwenye mtungi huo na mafunza yatakusanywa wakiwa wanaelea juu. Baada ya kukusanya waoshe vizuri na maji halafu lisha kuku moja kwa moja.

  5. g) Kumbuka kuweka chungu kinachooteshwa mafunza kuweka mbali na maeneo ya watu ili kuepuka harufu inayoweza kusumbua watu.


                                                  KULISHA KUKU:  
 

Makadirio ya chakula cha kuwalisha vifaranga 100/siku moja:






































Umri (wiki baada ya kuzaliwa)Idadi ya

vifaranga
Kiasi kinachotakiwa

Kwa siku moja(kilo)
11001
21001
31002
41003
51004
61005

Maelezo kwa ufupi  kuhusu kulisha kuku:

  • Ni vigumu kukadiria mahitaji ya chakula cha kuku wanaojitafutia chakula, lakini inakadiriwa kuwa kuku mmoja mkubwa wa uzito wa kilo 1-2 anahitaji chakula chenye uzani wa gramu 80-160 kwa siku kwa kuku wanofugwa ndani lakini wale kuku wanafugwa kwa mfumo wa huria nusu huria mahitaji yanakadiriwa kupungua hadi kufikia gramu 30-50 kwa siku .

  • Ifahamike pia kuwa kiasi cha chakula hutegemea mahitaji kutokana na uzito na uzalishaji, mfano kuku anayetaga na anayekua wanahitaji chakula kingi zaidi ya wale ambao hawatagi au wamekoma kukua.

  • Hakikisha kuku wanawekewa chakula na maji safi kwenye vyombo safi na kubadilisha kila vitakapoisha.

Jumanne, 23 Mei 2017

Mtaji wa kufuga kuku wa kienyeji, mchanganuo wake na namna ya kupata soko


Pengine umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Yako mambo mengi ya kufanya mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
Somo langu ni dogo lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana. Sasa kuwa makini zaidi.

Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

 

Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

 

vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri.

 

Wale vifaranga tunakadiria kuwa makoo(majike) watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

 

Utakuwa na kuku 200 + 25 =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu mfuatiliaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku 1,000. Miaka 2. 750(majike) x 10 = 7500 (uza wengine) 3000 x 10 = 30,000. Kutegemea na uwezo wako mpaka mwisho wa mwaka wa pili utakuwa umefanikiwa sana.

Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

 

  1. Kumbuka kuku ninao wazungumzia hapa ni wale wa kawaida wa kienyeji.Fuatilia zaidi kuhusu matibabu na matunzo mengineyo.


.

A.KWA NINI KUKU WA KIENYEJI?

  1. Wastahimilivu wa magonjwa lakini ni muhimu wakikingwa na magonjwa ya kuku kama mdondo, ndui ya kuku n.k ili kuweza kuwaendeleza.
    2. Wana uwezo wa kujitafutia chakula ardhini.
    3. Wana uwezo wa kuatamia mayai, kutotoa na kulea vifaranga na ustahimilivu wa mazingira magumu kama ukame, baridi n.k
    4.Nyama na mayai yake vina ladha nzuri kuliko kuku wa kisasa.(PATA SUPU YA KUKU WA KIENYEJI ILI UTHIBITISHE)
    5. Wana uwezo wa kujilinda na maadui kama mwewe n.k . Pamoja na sifa hizi ni muhimu muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri, wakawekwa kwenye mabanda mazuri, wakapewa maji na chakula cha kutosha.


B.FAIDA ZA KUKU WA KIENYEJI.

Faida ni nyingi na zinafahamika lakini nitaeleza zile ambazo kwa wengine huenda zikawa ni ngeni kwao.
- Mayai huweza kutumika kwa tiba. (Pata maelezo jinsi yai la kuku wa kienyeji linavyoweza kutumika kwa tiba kutoka kwa wataalam wa tiba mbadala)
- Kiini cha njano cha yai kinaweza kutumika kutengenezea mafuta ya nywele (shampoo)
- Manyoya yake yanaweza kutumika kama mapambo.
Fuga kuku upate faida kwa kuzingatia:
Chanjo ya mdondo kila baada ya miezi mitatu na chanjo ya ndui mara mbili kwa mwaka
Zuia viroboto, utitiri na minyoo.
Chagua mayai bora kwa ajili ya kuatamiza
Panga kuuza kuku kwa makundi uongeze kipato
Kula mayai na kuku kadri uzalishaji unavyoongezeka.
Kipato unachokipata utenge pia na kiasi kwa ajili ya uendelezaji wa kuku

C:MAPUNGUFU

Yako mapungufu mengi yanayofahamika lakini hapa naomba niweke lile la muhimu zaidi. MAGONJWA kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku kutokana na kutokuzingatia kuchanja kuku kwa wakati.

 

D: KABILA ZA KUKU WA KIENYEJI

Kuna maelezo ya kusisimua sana kuhusu makabila ya kuku wa kienyeji, hata hivyo kuna ugumu kidogo kuweza kuyachanganua makabila hayo kutokana na muingiliano mkubwa wa vizazi kati ya aina mbalimbali za kuku hao. Hata hivyo kuku hawa wana tofauti za kimaumbile zinazosaidia kwa kiasi fulani kutambua uwepo wa baadhi ya makabila ya kuku. Kabila hizi pia zinahusishwa kwa kiasi kikubwa na eneo kuku wanakotoka. Baadhi ya kuku wa kienyeji wanaweza kutambuliwa kwa maumbile yao Mfano:

  1. Kishingo - kuku wasio na manyoya shingoni
    b. Njachama au Nungunungu - Hawa ni wale wenye manyoya yaliyosimama.
    c. Kibwenzi - Ni wale wenye manyoya mengi kichwani.
    d. Kibutu- Hawa hawana manyoya mkiani
    Mwingiliano wa vizazi unaweza ukasababisha kuku kuwa na aina ya maumbile mchanganyiko. Mfano kuku aina ya kuchi anaweza kuwa na alama ya kishingo, Njachama, Kibwenzi au Kibutu.


Hivyo kabila za kuku zifuatazo zinaweza kutambuliwa kama ndiyo kabila za kuku wa kienyeji kulingana na maumbile yao na maeneo wanakotoka.

(i)          KUCHI
Ni kuku warefu kwa umbo na wenye kusimama mgongo ukiwa wima. Wana manyoya machache mwilini na hasa kifuani, vilemba vyao ni vidogo. Majogoo huwa na wastani wa uzito wa Kg. 2.5 na mitetea kg 1.5 mayai ya kuchi yana uzito wa wastani wa gm 45. Kuku hawa hupatikana kwa wingi maeneo ya Mwanza, Shinyanga, Tabora na Zanzibar.

(ii) CHING'WEKWE

Kuku hawa ambao jina lao ni gumu kidogo kwa mtu asiyekuwa na meno kulitamka wana sifa zifuatazo.
Majogoo wana wastani wa kg 1.6, Mitetea wastani kg 1.2, mayai wastani wa gm 37. Kuku hawa wenye umbo dogo hupatikana zaidi maeneo ya CHAKWALE mkoani Morogoro na pia sehemu za umasaini. Kuku hawa hutaga mayai mengi sana kuliko aina nyingine ya kuku wa kienyeji waliopo Tanzania, kwa hiyo wanafaa sana kwa biashara ya mayai.

(iii)UMBO LA KATI

Majogoo wana uzito wa wastani wa kg. 1.9, Mitetea kg. 1.1, Kuku hawa ndio hasa wanaoitwa wa kienyeji(wa kawaida) Wana rangi tofauti. Utafiti umeonyesha kuwa kuku hawa hukua upesi na hupata kinga upesi baada ya kuwachanja dhidi ya ugonjwa wa mdondo (Castle desease)
Muhimu - Mfugaji akifanya uchaguzi kutoka kwenye aina hii ya kuku na kutoa matunzo mazuri kwa hao kuku waliochaguliwa, Hakika anaweza kupata kuku walio bora na wenye uzito wa kutosha pia kutaga mayai mengi na makubwa.

(iv) SINGAMAGAZI

Ni aina ya kuku wakubwa wa kienyeji wanaopatikana zaidi TABORA, kuku hawa wana utambulisho maalum kutokana na rangi zao. Majogoo huwa na rangi ya moto na mitetea huwa na rangi ya nyuki. Uzito - Majogoo uzito wa wastani wa kg 2.9, mitetea wastani wa kilo 2 mayai gramu 56.

(v) MBEYA
Kuku hawa wanapatikana Ileje mkoani mbeya. Asili hasa ya kuku hawa ni kutoka nchi ya jirani ya Malawi na si wa kienyeji asilia bali wana damu ya kuku wa Kizungu "Black Australop". Majogoo Kg 3 mitetea kg 2 mayai gram 49

(vi) PEMBA
Hupatikana zaidi Pemba. Majogoo Kg.1.5 Mitetea Kg 1 mayai wastani gm 42

(vii) UNGUJA.
Majogoo Kg 1.6, mitetea kg 1.2 mayai gm 42. Kuku hawa wa Unguja na Pemba wanashabihiana sana na Kuchi isipokuwa hawa ni wadogo.

Jumamosi, 13 Mei 2017

Dume Mzuri Kwa Uzalishaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa


http://ufugajimakini.blogspot.com/

Tunaangalia uchaguzi wa dume mzuri kwa uzalishaji wa ng’ombe wa maziwa, pamoja na aina ya malisho ambayo mfugaji anaweza kuyatumia kuweza kukabiliana na changamoto ya malisho kwa ng’ombe.
Wafugaji wengi wamekuwa wakipata ng’ombe wanaozalisha kidogo na kwa kiwango cha chini kutokana na kuangalia ukubwa wa gharama ya mbegu wakidhania kuwa ndiyo upatikanaji wa ng’ombe bora. Vinasaba husaidia kwa kiwango kikubwa katika kupata ng’ombe mzuri wa maziwa.



http://ufugajimakini.blogspot.com/

Kuwepo kwa ongezeko la uzalishaji wa maziwa hutegemeana na vitu viwili ambavyo ni kuboresha mifugo kwa kufanya uchaguzi sahihi wa kizazi pamoja na usimamizi mzuri unaojumuisha lishe kamili, malazi mazuri, upatikanaji wa maji,kuwa karibu na wanyama pamoja na utoaji wa kinga na tiba dhidi ya magonjwa.



Vinasaba pamoja na usimamizi mzuri ni vitu viwili vinavyotegemeana. Bila kuwa na uzao mzuri, uzalishaji wa wanyama pamoja na usimamizi utakuwa wa hali ya chini sana, na bila usimamizi mzuri wanyama bora hawawezi kuonesha ubora wao katika uzalishaji.



Uzao mzuri humpa nafasi kubwa mfugaji kutambua sifa na uzalishaji utakaopatikana katika uzao ujao. Endapo mfugaji atafanya uchaguzi mbaya basi ni hakika atakuwa na uzalishaji hafifu wa maziwa, kuzorota kwa afya ya mnyama pamoja na maisha mafupi.



Muda wa kufanya tafiti



Wafugaji wengi wamekuwa wakifikiria mbegu pale tu ng’ombe anapokuwa tayari anahitaji kupandwa na matokeo yake ni kuwa, kutokana na haraka ya kutaka kumhudumia ng’ombe huyo, basi mfugaji atakuwa tayari kuchukua mbegu yoyote ile atakoyopatiwa na wataalamu. Kwa mantiki hiyo, hakuna muda mfugaji atatumia kuchunguza aina ya dume aliyetumika kupatikana kwa mbegu hiyo na badala yake, gharama hutumika kwa kiasi kikubwa kuonesha uwezo wa dume huyo.



Wafugaji wengi hufikiri kuwa kitendo cha mbegu kuuzwa kwa gharama kubwa ni moja ya njia ya kutambua ubora wa dume. Wauzaji wengi wamekuwa wakitumia njia hii kuwadanganya na kuwarubuni wafugaji.



Ni muhimu sana kwa mfugaji anaelenga kuzalisha maziwa kusoma na kuelewa taarifa zote muhimu zilizotolewa kuhusu aina ya dume husika. Ili kufanikiwa katika uzalishaji wa maziwa, ni muhimu kwa mfugaji kuwa makini na kulichukulia kwa uzito suala la uchaguzi wa dume na kuelewa nini kinahitajika bila kubahatisha. Mfugaji ni lazima atambue kuwa, dume huchangia asilimia 50 ya kinasaba katika uzao wake hivyo ni muhimu sana kujua sifa za dume unayemchukua kwa ajili ya uzalishaji. Pia ubora wa maziwa huchangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya dume aliyetumika. Dume wa maziwa hutambulika kwa kuangalia kiwango cha maziwa yanayozalishwa na ng’ombe aliyepandwa na dume huyo na mtamba aliyezaliwa na ng’ombe huyo ambapo dume huyo husambaza sifa ya maziwa kutoka kwa ng’ombe huyo hadi kwa mtamba.



Elewa maelekezo yaliyopo kwenye kabrasha la mbegu



Kielelezo cha vinasaba hutumika kupima uwezo wa mnyama kusambaza vinasaba vyake kwenda kwa uzao ujao. Katalogi huwa na taarifa muhimu ambazo zitamsaidia mfugaji kufanya uchaguzi mzuri wa dume ili kuwa na uhakika wa kuendeleza kizazi baada ya kingine.


Jumatano, 26 Aprili 2017

NJIA BORA ZA UTUNZAJI WA MAYAI YA KUKU


Kwa kawaida kuku huanza kutetea(Kutoa mlio wa ishara ya kutaga) anapofikisha miezi sita hadi minane. Hivyo ni vyema viota viandaliwe mapema wakiwa na umri wa miezi mitano. Kuku anapoanza kutaga akifikisha mayai matatu mfugaji anashauriwa kuondoa kila yai linalozidi hayo matatu kila siku linapotagwa na kuliweka alama ya tarehe au namba kwa kutumia penseli ili kumfanya kuku aendelee kutaga kwa lengo la kufikisha mayai 15 mpaka 20. Mayai yanayoondolewa yawekwe kwenye chombo kikavu kinachopitisha hewa ni vizuri pia kuweka mchanga ndani ya chombo hicho.

Hakikisha ya fuatayo.
Sehemu iliyochongoka iwe chini na pana iwe juu.
Hifadhi sehemu yenye hewa ya kutosha na isiyohifadhi joto
Mayai yasikae kwenye hifadhi hiyo zaidi ya wiki mbili toka siku ya kuanza kutagwa.

UATAMIAJI WA MAYAI NA UANGUAJI WA VIFARANGA
Uatamiaji na uanguaji wa kubuni - Mfumo huu hutumia mashine za kutotoleshea vifaranga (Incubators) hutumika kuangua mayai mengi kati ya 50 hadi 500 kwa wakati mmoja Mashine zinazotumika kutotoleshea vifaranga wa kisasa zinaweza kutumika pia kutotoleshea wa kienyeji.
Uatamiaji na uanguaji wa asili

KUCHAGUA MAYAI YA KUANGUA.
Hili nalo ni muhimu kuzingatia. Ni vizuri kuchagua mayai ya kuatamia ili mayai yasiyofaa yaweze kuuzwa au kutumiwa nyumbani kwa chakula. Mayai ya kuatamia yawe na sifa zifuatazo
Yasiwe na uchafu yawe masafi
Yasiwe na nyufa
Yatokane na kuku aliyepandwa na jogoo
Yasiwe madogo wala makubwa bali yawe na ukubwa wa wastani kulingana na umbile la kuku.
Yasiwe mviringo kama mpira pia yasiwe na ncha kali sana.
Yasiwe yamekaa muda mrefu zaidi ya wiki mbili toka yalipotagwa
Yasiwe yaliyohifadhiwa kwenye sehemu yenye joto.

KUMTAYARISHA KUKU WA KUATAMIA
Pamoja na matayarisho hayo zingatia kumuwekea mayai yasiyozidi 15 pia ni vizuri yasipungue 12. Kuku wanaotazamiwa kuatamia ni lazima wachunguzwe kwa makini kabla ya kuatamia ili kuhakikisha kwamba hawana chawa, utitiri n.k. Kuwepo kwa wadudu hao huwafanya kuku wakose raha na kutotulia kwenye viota vyao. Hali hii husababisha kuanguliwa kwa Vifaranga wachache.
Sasa unatakiwa kufanya yafuatayo:-
Nyunyiza dawa ya kuua wadudu ndani ya kiota
Pia mnyunyuzie dawa kuku anayetarajia kuatamia
Weka mayai kwenye kiota huku mikono yako ikiwa imepakwa jivu ili kuepuka kuwa na harufu kwani kuku anaweza kuyasusa.

Ni vizuri kuifanya kazi hii ya kumuandaa kuku anayetaka kuatamia wakati wa usiku. Pia ifahamike kuwa kwa kawaida kuku huatamia mayai yake siku 21.

PIA JIFUNZE MBINU ZA KUATAMIA MAYAI MENGI KWA NJIA ZA ASILI.
Iwapo una kuku wengi wanaotaga kwa wakati mmoja ni vema ukawafanya wakaatamia na kutotoa pamoja.
Unachotakiwa kufanya ni kuchagua mayai ya kuatamia ukianzia na yai la mwisho kutaga.
Unaweza kuwaandaa kuku wako zaidi ya mmoja ili waanze kuatamia kwa pamoja na kupata vifaranga vingi kwa mara moja kuku wa kwanza anapoanza kuatamia. Mwekee mayai viza au ya kuku wa kisasa kwani kuku huatamia hadi mayai yanapoanguliwa hivyo ukimuwekea mayai yasiyo na mbegu atakaa hapo muda mrefu hadi vifaranga watoke.

UTEKELEZAJI WAKE.
Kuku anapotaga kila siku weka alama ya namba au tarehe kulinganisha na siku anayotaga
Yanapofika mayai matatu yaondoe na muwekee mayai viza au ya kisasa huku ukiendelea kuweka alama mayai yanayotagwa kila siku.
Mara kuku anapoanza kuatamia muongezee mayai ya uongo yafikie 8 hadi 10
Fanya hivyo kwa kila kuku anayetaga hadi utakapoweza kupata idadi itakayoweza kukupatia vifaranga wengi kwa wakati mmoja.
Wawekee kuku wote mayai siku moja kwa kuondoa mayai ya uongo na kuwawekea mayai ya ukweli wakati wa usiku.

MUHIMU.
Mayai ya kuatamia yasishikwe kwa mkono ulio wazi na wala yasipate harufu za mafuta ya taa, manukato n.k.

JIFUNZE PIA KUTAMBUA MAYAI YALIYO NA MBEGU NA YALE YASUYO NA MBEGU.
Mfugaji anaweza kutambua mayai yaliyo na mbegu na yale yasiyo na mbegu siku ya saba baada ya kuanza kuatamia iwapo atapima mayai kwa kutumia box lililotengenezwa maalum pamoja na tochi yenye mwanga mkali ndani ya chumba chenye kiza. Hii itamuwezesha mfugaji ayatumie mayai yasiyo na mbegu kwa chakula cha familia au kuyauza.

UTUNZAJI WA VIFARANGA(KUKU WA KIENYEJI NA WA MAYAI)


Utunzaji wa vifaranga:- siku ya kwanza waweke katika brooder(banda la kuku)wape glucose kwa masaa sita hadi nane ya kwanza kurudisha nguvu iliyo potea
baada ya kuwapa glucose wape Esb3 au S-dime au amprolium kwa siku 1-3
Siku ya 3-5 wape chick formula,Siku ya 6 wape maji peke yake,siku ya 7 wape NCD vaccine(New castle)kwa muda wa masaa 2 tu kasha wape maji yenye vitamins,siku ya 10 wape chanjo ya gumboro,siku ya 13 wape typhoprim na neoxyvital kwa muda wa siku 7 kisha wape vitamin na dawa hizi kila mwezi kwa siku tatu
b)Utaratibu wa kuwapa chanjo:- siku ya 7 wape new castle,siku ya 10 wape chanjo ya gumboro,siku ya 21 rudia kuwapa chanjo ya gumboro,siku ya 42 rudia new castle kasha rudia kila baada ya miezi 3
c)Minyoo:-Wape dawa ya minyoo wanapo fikia umri wa wiki 8 na rudia kila baada ya miezi 3
d)Magonjwa:- Chunguza tabia ya kuku kama wanakula vizuri na wanakunywa maji vizuri na ya kutosha, wanatembea vizuri na wanachangamka sikiliza sauti zao angalia mwenendo wa ukuaji wao na mwenendo wa utagaji angalia kila siku vifo vinavyo tokea bandani,ukiona mabadiliko yasiyo ya kawaida mwone mtaalam wa mifugo aliye jirani na ulipo
Upatikanaji wa vifaranga:-
Magonjwa ya kuku:- Occidiosis ugonjwa wa kuharisha hutokana na uchafu bandani au mazingira yanayo zunguka banda,wasambazaji wa ugonjwa huu ni kunguru(mwewe)ndege wanao kuja eneo lenye kuku ,panya n.k
Kutibu ugojwa huu wape amprolium au dawa ya typhoprim na neoxyvital(vijiko 2 vya chakula kwenye maji yenye ujazo wa lita 20 kwa siku 14
Kuku wanapo ambukizwa coccidiosis ni rahisi kupata typhoid ukigundua kuku wako wameambukizwa (wanaugua typhoid )wape typhoprim 30% pamoja na ctc20% au otc 20 na vitamin amilyte
Chakula kilicho tengenezwa kutumia dagaa na samaki kinachangia kuongeza kusambaa kwa ugonjwa wa typhoid kwa kuku,epuka kuwapa kuku chakula chenye samaki na dagaaa,wape maharage ya soya au mashudu ya alizeti,kuku wakiwa wanachechemea(miguu kukosa nguvu) ni kutokana na upungufu wa chokaa
Kuku wanao anza kutaga:-wape typhoprim30% na neoxyvital siku 5-7
Usafi wa banda
Baada ya kubadilisha maranda au pumba za mpunga zilizopo kwenye banda ongeza pumba za mpunga pindi ukiona zime anza kuwa chafu ugojwa ukiendelea muone mtaalam wa mifugo aliye karibu yako

MPANGILIO WA CHAKULA CHA KUKU WA KIENYEJI
Kuku wa kienyeji wanafugwa kwa sababu hutupatia kitoweo na pia hutupatia mayai na kipato kwa familia na maranyingi vifaranga wa kuku wa kienyeji hufugwa kama vifaranga wa kuku wa mayai na wa nyama
Vifaranga wenye umri wa kuanzia siku 1 hadi wiki 3-4 asipewe chick starter
Kuku wenye umri wa wiki nne huitwa mitemba kuku wa umri huu wanahitaji chakula maalum,kuanzia wiki 5-8 wapewe chick mash kuanzia wiki ya 9-17 wapewe growers mash mabadiliko yasifanyike ghafla changanya chakula cha kukuzia na kutagia.Pia unaweza kuwapa mtama mweupe au uwele na mashudu ya alizeti kutokana na kupanda kwa bei za chakula.
UJENZI WA BANDA LA KUKU(BROODER)HADI MIEZI MIWILI
Banda lenye uwezo wa kulea vifaranga 100
Banda liwe na urefu wa futi 10 upana futi 10
Kutoka msingi hadi kufikia madirisha(ventilation space)kozi nne jengea wavu wa kuku kwa ajili ya hewa urefu wa kwenda juu uwe mita 1 pia unaweza kujengea mabanzi
Urefu wa banda kwenda juu usupungue futi 10
Paa lake liwe imara lisilo vuja
Sakafu iwe imara
Mlangoni tengeneza kikaro kidogo kwa ajili ya kuweka dawa ya kuzuia magonjwa(disinfectant).
KUWEKA MARANDA AU PUMBA ZA MPUNGA
Weka ujazo wa inchi 2 katika banda la kulea vifaranga
VIPASHA JOTO NDANI YA BANDA
Tumia umeme hakikisha bulb ipo katikati zina takiwa ziwe mbili zenye W 100,umeme ukikatika tumia kandili 2 au 3 kubwa.Pia unaweza kutumia jiwe la mkaa weka juu ya tofali la nchi 5 tumia mkaa usio toa cheche na usio isha haraka .
Siku 4 au saba kabla ya kuingiza vifaranga andaa mambo yafuatayo
Kung’utia dawa ya kuua wadudu(viroboto au utitili
Tandika makaratasi au magazeti juu ya maranda
Kwenye madirisha hakikisha unaweka mapazia ya viroba au yasiyo shika vumbi
Hakikisha umeandaa pesa za kununulia chakula cha kuku,vyombo vya kunyweshea na kulia chakula pamoja na madawa.
MADAWA:-

OTCPLUS20%(KUKAUSHIA VITOVU)
VITAMIN(KUONGEZA VITAMIN)
GLUCOSE(KUONGEZA NGUVU HARAKA)
VIPIMO:-Dawa zote ,chukua maji safi na salama lita 5 kila dawa chota kijiko cha chai(grm5)weka kwenye lita 5 za maji kwa siku 5 watakunywa mchanganyo huo baada ya siku 5 wape maji safi na salama(bila dawa)
KUPOKEA VIFARANGA:- Masaa 12 kabla ya kupokea vifaranga hakikisha brooder lina joto la kutosha ili vifaranga wafikie katika joto zuri
Hakikisha umechanganya dawa zilizo tajwa hapo juu pia umeandaa chakula
Wanapo fika vifaranga hakikisha wameanza kunywa maji yenye dawa baada muda kidogo wape chakula(kumbuka kuwachanja kabla ya msimu wa mvua na baada ya msimu)
MAHALI PA KULALA KUKU WAKATI WA USIKU(PERCH-SPACE)
Kuku wapatiwe sehemu ya kulala au kupumzika
KINGA YA MAGONJWA(VACCINATIONS)
Wapewe new castle vaccine siku ya saba
Wapewe gomboro siku ya kumi na nne
Wapewe Fowl pox(ndui)baada ya wiki 8
Wapewe dawa ya minyoo mwanzoni mwa msimu wa mvua na mwishoni mwa msimu wa mvua
Usafi ni muhimu
Tanbihi:-Ni vyema kuhifadhi kumbukumbu kila unapo wapa chanjo
KUPANDA NA KUSHUKA KWA JOTO:-

Utakapo ona vifaranga wame samba punguza joto bandani
Na utakapo ona vamejikusanya ongeza joto bandani
MEDICATION

(Kutibu):- matibabu huwa baada ya uchunguzi wa daktari wa mifugo(vet officer)
Njia za kutibu:-kuwapa kwenye maji(make a cream)
Kuwapa kwenye chakula(make a premix)
Kwa njia ya kuchoma sindano(wing wabe),breast muscles(intramuscle)
Kupuliza(spray method)
Vifaranga hukoma kuwa vifaranga wafikiapo wiki nane

NJIA BORA NA YENYE KULETA TIJA KWA WAFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI
Kuchagua kuku wa kufuga:-aina za kuku wazuri-kuchi na bukini hutaga na kuatamia mara 10 kwa mwaka,hutaga kwa wingi na kwa haraka na wana faida kubwa na mtaji wake ni rahisi kwani unaweza kuanza na jogoo 1 na koo(tetea) 1au 2 na ili kuleta tija una shauriwa kuwatunza kuku vizuri
Ushauri:-mfugaji asiwaa chie kuku kuzurura sana(itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya kuambukizwa na kuku wa jirani,mfugaji aweke uzio japo kidogo na si lazima shamba lote.Mfugaji anatakiwa aongeze vifaranga vitakavyo kua kwa kulea vifaranga mwenyewe
Dawa za kupuliza kwenye banda la vifaranga ni servin powder au akheri powder

Aina ya Vyakula Kiasi(kilo)

Magimbi,mihogo,mahindi au uwele(paraza) 40kg
Pumba za mahindi,uwele,ngano au mpunga 27kg
Mashudu ya alizeti,pamba ufuta,karanga,nazi,soya au mawese. 20kg
Unga wa mifupa,chokaa au magamba ya samaki baharini yaliyo sagwa 2.25kg
Dagaa au mabaki ya samaki
Chumvi ya jikoni 0.50kg
Virutubisho(premix) 0.2.5kg
jumla 100kg

Makadirio ya mahitaji ya chakula kwa siku kulingana na umri
umri Kiasi(grm)
Wiki ya kwanza

1 12-15
2 15-21
3 21-35
4-7 35-50
8-15 55-60
Mchanganyiko wa chakula cha kuku wanao kua na kutaga
kg kg kg kg
Malighafi inayotumika 1 2 3 4
Mahindi yaliyoparazwa 45 20
mtama 5 30
mihigo 20 10 40
Pumba za ngano 15 15 10
Pumba za mahindi 15 15 15 20
Mashudu ya alizeti 16 16

Mashudu ya pamba 3 5
Maharage/kunde zilizo sagwa 1 5 3.5 1
kisamvu 4.75
Lusina/lusani iliyo sagwa 1 5 5 2
chokaa 5 6 4 5
Dagaa au sangara 6 5 5
Mifupa iliyo sagwa 2.25 2.25 2 2
Damu iliyo kaushwa 1 5 3.25
Chumvi ya kausida 0.50 0.50 0.50 0.50
Vitamin/madini(premix 0.25 0.25 0.25 0.25
jumla 100 100 100 100

Ijumaa, 21 Aprili 2017

FAHAMU KILIMO BORA CHA MIHOGO CHENYE TIJA

Zao la muhogo ni  muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini. Wakulima wengi huchanganya zao la muhogo na mazao mengine kama vile kunde, mbaazi, njugumawe, n.k. Umuhimu wa zao hili ni kutupatia cahakula na wakati mwingine kwa biashara. Kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula kikuu ambacho kinachukua asilimia 75 ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya pwani.

Muhogo hustawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye maeneo ya mita 0 – 1500 kutoka usawa wa bahari. Vile vile muhogo hustawi vizuri kwenye maeneo yanayopata mvua ya wastani wa mm 750  - mm1200 kwa mwaka. Muhogo hustawi vizuri kwenye ardhi ya kichanga. Vili vile zao la muhogo ni maarufu sana kwa uvumilivu wa hali ya ukame.

TEKNOLOJIA ZILIZOPO
Mbegu bora za muhogo
Mpaka sasa hivi kuna aina mbili za mbegu bora ambazo zimathibitishwa kwa wakulima. Mbegu hizi huvumilia magonjwa, (batobato na matekenya), pia huzaa sana ukilinganisha na mbegu za kienyeji.
Naliendele Huzaa tani 19 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

Kiroba
Huzaa tani 25 – 30  kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9toka ipandwe.

Mbinu bora za kilimo cha muhogo
Uandaaji wa shamba
Shamba liandaliwe kabla ya msimu wa kuanza. Uandaaji wa shamba bora hufuata hatua zifuatazo:

  1. Kufyeka shamba

  2. Kung’a na kuchoma visiki

  3. Kulima na kutengeneza matuta

  4. Uchaguzi wa mbegu bora za kupanda

  5. Mbegu zinatakiwa zisiwe na magojwa yeyote, pia chagua mashina ambayo yamelomaa vizuri.

  6. Upanadaji

  7. Kuna njia tatu za upandaji wa muhogo:

  8.  Kulaza ardhini (Horizontal)

  9.  Kusimamisha wima (Vertcal)

  10. Kuinamisha ( Inclined/Slunted)


Urefu wa kipande cha shina cha kupanda:
Inashauriwa urefu uwe sm 30; lakini urefu wa kipande cha kupanda unategemea sana idadi ya macho yaliyopo kwenye hicho kipande, inashauriwa kipande kiwe na macho (4 – 6).

Nafasi ya kupanda:
Kwa upandaji wa shamba muhogo tupu, shina hadi shina ni mita 1 na mstari hadi mstari ni mita 1.Kwa shamba la mchanganyiko na mazao mengine, inategemeana na zao linalochanganywa; mstari hadi mstari ni mita 2 – mita 4 na shina hadi shina ni mita 1.

Palizi:

  •  Palizi ya kwanza ifanyike mapema (mwezi 1) baada ya kupanda ili kuepukana na magugu yanayochipua haraka baada ya mvua kunyesha. Ndani ya miezi mine ya mwanzo mihogo haitakiwi kuwa na magugu ili kuepuka ushindni wa mahitaji muhimu (mwanga, mbolea, maji, n.k) kati ya muhugo na magugu.

  •  Palizi hufanyika kwa kutumi jebe la mkono au dawa ya kuuwa magugu.

  • Wakati mwingine udhibiti wa magugu kufanyika kwa kutumia majani kwa kutandazwa juu ya udongo.

  • Plaizi hufanyika mara 2 – 3 hadi muhugo kukomaa.



Uvunaji:
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 – 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvuna katika katika kipindi cha jua; kwani wakati wa mvua kiwango cha wanga kwenye muhogo hupungua.

Usindikaji bora
Usindikaji bora wa muhogo unafanyika kwa sababu kuu mbili:

  • Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji

  • Kuondoa sumu (cyanide) ilyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo

  • Kuongeza ubora wa unga utokanao muhogo wenyewe.


Njia bora za usindikaji

  • Kwa kutumia mashine aina ya Grater

  • Hii hutoa chembechembe laini za muhogo, ambazo baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kingine kiitwacho “presser” ili kuondo sumu iliyoko kwenye muhogo. Mashine hii hutumika hususani kwa muhogo mchungu.

  • Kwa kutumia mashine aina ya chipper

  • Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo (chips). Mashine hii hutumika hasa hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.


Matumizi ya Muhogo

  • Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga

  • Unga wa muhogo unaweza kutengeneza vitu vyotekama vinavyotengenezwa na unga wa ngano kama vile biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k.

  • Pia muhogo huweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa nyingine kama vile wanga.


iii MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
Magonjwa
Kuna magonjwa mawili ambayo ni muhimu sana na yanapunguza uzalishaji wa zao la muhogo.

a) Ugonjwa wa Matekenya au Ugonjwa wa michirizi ya kahawia katika muhogo
Ugonjwa huu ni maarufu kwenye sehemu zenye miinuko iliyo na urefu  chini ya mita 300 na unapatikana kidogo sana kwenye miinuko ya mita 500 na kuendelea ambako uenezaji wake wa kawaida hautokei kabisa.

Visababishi:
Matokeo ya uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba ugonjwa huu ulienezwa na mdudu mweuupe au inzi mweupe (whitefly) mwenye mabawa madogo.

Dalili za Ugonjwa
Sehemui zote za muhogo zinaweza kuonyesha dalili za uambukizo wa ugonjwa huu lakini ni vipengele gani vya ugonjwa na ni kwa kiwango gani hutegemea hali ya mzingira, hatua ya kukua kwa mmea kwa kulinganisha.

Kwenye majani

  • Dalili ya kwanza: Chlorosis rangi ya njani hutokea kwanza pembezoni mwa vena ndogo baadae huathtiri vena ndogo zaidi na inaweza kuwa doa (chlorosis) la rangi ya njano.

  • Dalili ya pili: Rangi ya njano ambayo haihusishwi vizuri na vena isipokuwa katika mbaka ya mviringo kati ya vena kuu kwenye hatua za mwisho za ugonjwa sehemu kubwa ya lamin inaweza isiathirike, majni yenye ugonjwa hubaki yameshikilia kwenye mmea kwa muda wa wiki kadhaa.


Kwenye shina
Huonekana kwenye tisu ya shina changa la kijani, jeraha la zambarau au kahawia linweza kuoneakan nje na kuingia ndani hadi kwenye gamba baaada ya kubandua gome la nje. Pia jeraha la nekrotiki kwenye kovu la shina hutokea baada ya majni kudondoka kutokana na umri wa mmea. Tawi/shina hufa kuanzia kwenye nch kuelekea chini na kusababisha kufa kwa mmea wote.


Kwenye mizizi

Kwa kawaida hutokea baada ya dalili za majani na wakati wa kipindi kati ya uambukizo na kufa, amabpo kifo cha mizizi hutokea kuanzia miezi 5 toka kupandwa. Dalili za mizizi zinabadilika nje ya mizizi na zinaweza kuwa kamakizuizimwanga au shimo au kufa kwenye gome.

Tishu inayo zunguka mshins ina doa la rangi ya kahawia au nyeusi. Wakati mwingine mizizi huonekana kuwa yenye afya kwa nje bila kuwa na matatizo yaliyowazi au bila kupungua ukubwa, lakini ikikatwa huonekana kufainakufa au rangi ya njano.
Uambukizaji na ueneaji

Ugonjwa wa CBSD unaambukizwa kwa njia ya vipandikizi vinavyotokea kwenye mimea iliyoathiriwa vinavyosababisha mmea kuonesha kwenye majani dalili za ugonjwa.

Kwa kuwa muhogo kwa kawaida huzalishwa kwa njia ya vipandikizi ugonjwa huu huingizwa kwenye sehemu mpya zilizopandwa kwa kutumia vipandikizi vilivyoambukizwa.
Kwa aina zinazovumilia sana kwenye hali za mabondeni, dalili mbaya sanahutokea wakati ugonjwa ukigundulika  katika hatua za mwanzo.

Uchunguzi umeonesha kwamba Bemisia afer ni mdudu/kisababishi ambacho ndicho kinachohusiana na maendeleo ya hivi karibuni kuhusu uhamishaji wa visababishi kama “ipomovirus”. Mara nyingine inaonesha nzi weupe (White flies) na kutokana na hali hiyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.

Udhibiti/Kuzuia

  • ü  Njia ya msingi ya kuzuia/kudhibiti ugonjwa wa CBSD ni kuchagua mbegu kutoka kwenye mimea isiyo na dalili ya ugonjwa.

  • ü  Ubora wa mashina unahitaji kutunzwa kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza ile iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.

  • ü  Hakikisha kuwa unapanda mbegu bora za mhogo ambazo zinastahimili uambukizo wa magonjwa.

  • ü  Hakikisha kuwa wakati wa uvunaji uonapo hali ya kuoza kwa mizizi ya mhogo ichome moto ili kutokomeza ugonjwa huo.

  • ü  Kuelewa dalili za ugonjwa wa CBSD kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya kutokomeza ugonjwa huu.

  • ü  Hakikisha kuwa unaendelea kutunza mbegu bora zinazoonekana kuvumilia magonjwa sana.

  • ü  Hakikisha kuwa shamba la mhogo linakuwa safi kwa ajili ya kupunguza visababishi vya ugonjwa wa CBSD

  •                                     


b) Ugonjwa wa batobato au ukoma wa majani
Ni ugonjwa ambao ulienezwa kwamara ya kwanza hapa Tanzani mwaka 1894, na baadae uliripotiwa katika nchi nyingine nyingi za Afrika Mashriki, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati na sasa unafahamika kuwa upo maeneo yote yanayolimwa muhogo Afrika.

Katika viwango vya kuwepo kwa ugonjwa wa CMD na katika uwingi wa hasara zinazopatikana kutokana na CMD ni kati ya 15% – 20%. Hii ni sawa na tani milioni 15 – 18 zikilinganishwa na makadirio ya shirika la kilimo na chakula  duniani ya tani milioni 85 ya mwaka 1997.

Visababishi
Tangu ugonjwa wa CMD ulipoenezwa kwa mara ya kwanza, visababishi vilichukuliwa  kuwa ni virusi kwa sababu ya kukosekana kisababishi kingine. Kwa hiyo kutokana na kuwa mtazamo huu unalingana na matokeo ya uchunguzi wa awali inaonesha kwamba ugonjwa huu huenezwa na nzi mweupe (white fly).

Pia uchunguzi wa mara kwa mara umesababisha utambuzi wa virusi vya aina mbalimbali na tofauti kama ifuatavyo:

  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Africa cassava mosaic virus

  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Afrika mashariki (East Africa cassava mosaic virus)

  • Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya India (Indian cassava mosaic virus)

  • Dalili za ugonjwa wa batobato (Cassava Mosaic Disease-CMD)


Dalili hutokea kwenye jani lenye uwaraza wa michirizi ambazo huathiri
Sehemu zisizokunjamana za kutolea hewa na hufahamika katika hatua za
Awali za ukuaji wa jani.

Sehemu za kloritiki hushindwa kutanuka hadi mwisho, hivyo mvutano unaji-
tokeza kutokana na ukuaji usiolingana na jani au majani madogo yaliyoharibika.
Majani yaliyoathirika sana hupungua ukubwa wa umbo, na hujikunja na kujitenga kwa
Sehemu zenye rangi ya njano na zenye rangi ya kawaida ya kijani.

Mmea hudumaa na majani machanga hupatwa na uvimbe.
Kloritiki ya jani inaweza kuwa ya rangi ya manjano nyepesi au rangi inayokaribia nyeupe
yenye kijani kidogo au kupauka kuliko ilivyo kawaida.


Uambukizaji na uenezaji

 

  • Ukoma wa mhogo huambukizwa kwenye vipandikizi vya shina ambavyo kwa kawaida

  • hutumika kuzalishia mmea.

  • Pia huenezwa na inzi mweupe (white fly) aitwae Bemisia tabaci G. Aina mbili za inzi au

  • Mbu hao Bemisia (Preisner Hhosny na Aleorodius disperses R) pia huambukiza mihogo

  • katika nchi za Afrika na India

  • Usambazaji wa vipandikizi unaweza kusababisha kuenea kwa ugonjwa wa CMD katika

  • Maeneo mapya.


UHIBITI NA KUZUIA

  • Hatua ya msingi ya uzuia ugonjwa wa CMD ni kwa kuchagua vipandikizi kutoka kwa Mmea ambao hauna uambukizo wowote.

  • Ubora wa mashina unahitajika kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza kwa kung’oa ile

  • Mihogo iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.

  • Hakikisha kuwa wakati wa kuvuna mihogo kwa ile iliyoathirika na ugonjwa wa CMD

  • inaangamizwa kwa kuchomwa moto.

  • Hakikisha una elimu ya kutosha juu ya dalili za ugonjwa wa CMD>


WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU

Cassava Mealy Bug (CMB)



Wadudu hawa hushambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani ynadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana.



Cassava Green Mites (CGM)
Wadudu hawa hushambulia majani mapya sehemu za chini. Madhara yake sio makubwa.



White Scales
Hawa ni weupe na hujishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo. Vili vile wadudu hawa madhara yake sio muhimu.

Mchwa
Hawa hutafuna/hula mashina ya muhogo hasa wakati wa jua kali/kiangazi.
Wanyama waharibifu
Hawa hushambulia muhogo ukiwa shambani kwa kuula, kama vile nguruwe, panya, wezi, n.k

Udhibiti/Kuzuia
Kwa upande wa wadudu wanweza kudhibitiwa kwa njia zifuatazo:
ü  Kutumia dawa za kuulia wadudu
ü  Kutumia wadudu marafiki wa wakulima
iii Kwa upande wa wanyama ni kuweka walinzi.

Jumatano, 19 Aprili 2017

AINA ZA NGOMBE WA MAZIWA


Ndugu msomaji leo nitakuletea kitu kipya na chenya manufaa sana ukikizingatia,hizi ni aina ya ng'ombe wa maziwa waliopo duniani

MAMBO YA KUZINGATIA KWENYE UCHAGUZI WA NG'OMBE MZURI WA MAZIWA

Umbo : siku zote ngo'mbe wa maziwa anatakiwa awe na umbola pembe tatu, humpless pia awe na miguu imara pamoja na tumbo kubwa kwa sababu ng'ombe mwenye tumbo kubwa anaweza kula sana na kutunza chakula kingi.na chakula kingine kinabadilishwa na kua maziwa.hivyo ng'ombe mwenye tumbo kubwa anauwezo wa kutoa maziwa mengi sana.

Kiwele na chuchu: siku zote ng'ombe mzuri wa maziwa anakiwele kizuri kimeshika vizuri kwenye mwili na kiwele kizuri hua kinabonyea kama spongy.na pia kiwele na chuchu vinatakiwa kua kubwa.

Rangi ya mwili : sikuzote ng'ombe mzuri wa maziwa anarangi moja au mbili tu kwenye mwili wake e.g brown, red white and black.

Asili : siku zote ng'ombe mzuri wa maziwa anatokea katika maeneo yenye hali ya hewa ya kati e.g Holland, Switzerland, Scotland and other part of Europe and Asia.

AINA ZA NG'OMBE WA MAZIWA

Kuna makundi mawili ya ng'ombe kuna wa nyama pamoja na wamaziwa. na kuna aina nyingine pia ni wazuri kwa nyama pamoja na wamaziwa mfano mpwapwa na sahiwal.

hizi hapa na aina za ng'ombe wa maziwa

  • Holstein Friesian



  • Brown swiss



  • Ayrshire



  • Guernsey



  • Jersey



  • Mpwapwa



  • Sahiwal



  • Red pollAINA ZA NG'OMBE WA MAZIWA NA SIFA ZAKE

    1.HOLSTEIN FRIESIAN

    Hii ni aina ya ng'ombe wa maziwa ambayo ni kubwa kuliko aina zote

    SIFA

    • Asili yake ni Holland



    • wanamabaka meupe na meusi



    • maziwa yao yana mafuta kiasi cha 3.5%



    • wanatoa maziwa mengi 6000 liters kwa kila msimu wa kukamua



    • watoto wake wanazaliwa wakiwa na 40 kg na zaidi.



    • jike anauzito wa 400-600kg na dume 600-1000kgs



    1. BROWN SWISS


    Hii ni kati ya aina za zaman sana, ili gunduliwa katika milima ya Switzerland?

    SIFA

    • Wame gunduliwa Switzerland



    • hii ni aina nzito inayo fuata baada Friesian



    • wanalangi ya brown inayo koza



    • niwapole



    • uzito wa jike 450-550kg na dume 600-900kgs



    1. AYSHIRE


    Hii ni aina kubwa inayo fata baada yaFriesian na brown Swiss

    SIFA

    Niwakubwa zaidi ya jersey na Guernsey

    wanarangi nyekundu kuelekea mahogany mchanganyiko na nyeupe

    asili yao ni South west Scotland

    maziwa yao yanamafuta 4%

    wanachuchu na kiwele kizuri sana

    1. Guernsey


    SIFA

    wanatoa maziwa yenye langi kama ya dhahabu

    wanarangi nyeupe na nyekundu

    maziwa yao yanamafuta 4.5%

    wanatoa maziwa 4200litres kwa msimu mmoja wa kukamua

    uzito wa jike 450-500kgs na dume 600-700kgs

    1. Jersey


    hii ndo aina ndogo kuzudi zote

    SIFA

    • asili yao ni visiwani kati ya UK na France



    • maziwa yao yanamafuta kuzidi wote 5%



    • wanarangi ya blackish brown



    • uzito wa jike 400-450kg dumeto 500-600kgs.


    asante mpenzi msomaji endelea kua na mimi upate kujifunza mengi kwa tasinia ya kilimo pamoja na ufugaj

Matumizi ya Mbolea


Matumizi ya rutuba kwenye udongo

  • } Mimea huchukua /huondoa virutubisho kutoka kwenye udongo kupitia kwenye mizizi.

  • } Virutubisho vinavyotumika na nafaka kama (ngano, mahindi, mpunga, n.k) inageuzwa kuwa punje na sehemu kwenye masalia ya mimea.

  • } Kwa upande wa mahindi ,kwa kila kilogramu 1000 ya mazao yanayozalishwa ,Kilogramu 35 za virutubisho zinakuwepo kwenye mazao na kilogramu 37 kwenye masalia  ya mimea.Jumla ya kilogramu 72 za virutubisho zinakuwa zimetoweka.

  • } Iwapo kwenye hekta moja umevuna tani 4 =kilogramu 4000, kiasi cha kilogramu 288 ya virutubisho itakuwa imeondolewa kutoka kwenye udongo.

  • } Kama hivi virutubisho havitarudishwa, rutuba ya udongo itapungua .Kwa miaka kadha wa kadha, mavuno kutoka kwenye udongo wa aina hiyo inashuka.

  • } Kwa udongo kubaki na rutuba, ni vizuri kurudisha virutubisho vilivyo potea wakati wa mavuno ya mazao.


Kutoka: IFDC: Estimated removal of nutrients from the soil by Grains (kg nutrients/ Mt grain harvested)































MimeaNitrojeni

(N)
Fosforasi

(P2O5)
Potasiamu

(K2O)
Jumla
Mahindi1810735
Ngano208533
Mpunga146424

Kutoka: IFDC: Estimated removal of nutrients from the soil by          Residue (kg nutrients/ Mt straw harvested)































MimeaNitrojeni

(N)
Fosforasi

(P2O5)
Potasiamu

(K2O)
Jumla
Mahindi1062137
Ngano632231
Mpunga922435

Virutubisho ni nini?

  • } Mimea inahitaji virutubisho kumi na sita ili kukua na kutoa maua na mazao mazuri.

  • } Virutubisho hutumika kama lishe ya mimea.

  • } Virutubisho vitatu hutoka hewani mambavyo ni: kaboni, oxijeni na hydrojeni.—Ikichangia asilimia 93 ya mahitaji ya mmea.

  • } Wakati virutubisho vitatu hutokana na hewa na maji .

  • } vingine kumi na tatu hupatikani kupitia udongoni.Hupatikana kupitia mizizi na kutumika na mimea.


Madaraja ya virutubisho vya mimea

  • } Kwa kuzingatia kazi zake na kiwango kinachohitajika na mimea kwa ukuaji kumetokea madaraja yafuatayo:



  1. Virutubisho vya msingi au vinavyohitajika kwa wingi



  • } Nitrojeni (N), Fosforasi (P), Na potasiamu (K) ndivyo vinahitajika mno na mimea kwa ukuaji na kwa kiwango kikubwa.



  1. Virutubisho vinavyo hitajika kwa kiasi



  • } Kalsiamu (Ca), salfa (S), and magnesiamu (Mg) huhitajika kwa kiasi kidogo na mimea lakini vinaumuhimu mkubwa.



  1. Virutubisho vinavyo hitajika kwa kiwango kidogo



  • } Virutubisho saba vilivyobaki ambavyo ni: Chuma (Fe), Kopa (Cu), zinki (Zn), boron (B), manganese (Mn), clorini (Cl), and molybdenum (Mo) huhitajika kwa kiwango kidogo sana.


Dalili kutokana na ukosekanaji wa vitutubisho Dalili kutokana na ukosekanaji wa vitutubisho

Virutubisho vya msingi

  • } Nitrogen (N), phosphorus (P), and potassium (K) ni vya aina tatu.


Kutokana na makubaliano ya vigezo vilivyowekwa na viwanda vya mbolea, virutubisho vya muhimu /msingi vimekubalika kama; N (nitrogen), P2O5 (or phosphorus pentoxide for phosphorus), and K2O (or potassium oxide for potassium

  1. Nitrogen

  2. Nitrojeni ndio kirutubisho cha muhimu kwa aina kubwa ya udongo unaonjesha mapungufu.

  3. Ijapokuwa Nitrojeni inahitajika katika ukuaji wa awali wa mimea ,inahitajika kwa kiwango kikubwa wiki ya 3-4 kutoka zao kuota haswa kwa mazao ya nafaka kama ngano,mahindi ,mpunga n.k.

  4. Nyongeza huwekwa baadae wakati mimea inapacha ,kutoa maua au karibu na kukomaa.

  5. Kwa hiyo Nitrojeni huwekwa kama mara 2-3 kwenye mimea


Dalili za mapungufu ya  Nitrojeni

  • } Kama nitrojeni imekosekane kwenye udongo:

  • } Ukuaji wa mmea huwa taratibu.

  • } Mmea hudumaa na majani kuwa ya njano.

  • } Mmea hukomaa haraka kupunguza mavuno.



  • } Upungufu wa  Nitrojeni

  • } Mapungufu ya nitrojeni hupatikana karibu kila eneo lakini zaidi kwenye udongo wa kichanga, udongo wenye kiwango kidogo cha mboji, au udongo uliolimwa mfululizo kwa miaka mingi.

  • } Aina ya mbolea inayotumika sana kusambaza nitrojeni ni mbolea ya Urea,SA,CAN



































MboleaVirutubisho %

N:P:K
Hutumika haswa
Urea46:0:0Kukuzia
Calcium Ammonium Nitrate(CAN)27:0:0Kukuzia
Sulphate of Ammonia(SA)21:0:0Kukuzia
Di -ammonia Phosphate (DAP)18:46:0Kukuzia
N:P:K17:17:17,20:10:10Kukuzia


  1. Fosforasi



  • } Fosforasi hupitia kwa mmea kwa kutumia mbolea za fosfeti,mara nyingi hutumika kupandia.

  • } Fosfati ni muhimu sana kipindi cha awali cha ukuaji wa mmea  kwa kuuwezesha mmea kuwa na mizizi mingi na kuwa na nguvu ya kuushikilia mmea kwenye udongo.

  • } Mizizi yenye afya huufanya mmea kupata vitutubisho kwenye udongo.


Dalili za mapungufu ya fosforasi

  • } Upungufu wa Fosforasi Huonekana haswa kwenye udongo wenye tindikali au ulio na kalsiuamu /chokaa kwa wingi.

  • } Mapungufu ya fosforasi kwenye udongo huufanya mmea kuwa :

  • } Dhaifu kutengeneza mizizi.

  • } Kuanguka kwa mmea.

  • } Kudumaa kwa mmea na mavuno kidogo.

  • } Mfano wa mbolea zenye Fosforasi ni: SSP (0-16-0),TSP (0-46-0),DAP (18-46-0)



  1. Potasiamu



  • } Potasiamu ni aina ya tatu ya kirutubisho cha msingi kinachohitajika na mimea.,barafu ,wadudu na magonjwa na kusaidia usafirishaji wa virutubisho vingine kuanzia kwenye mizizi hadi sehemu nyingine ya mimea.

  • } Inasaidia kujaza punje,mbegu.

  • } Mbolea zote zinazosambaza Potasiamu hutumika kupandia ila kwenye udongo wa kichanga inashauriwa kuwekwa mara mbili wakati wa kukuzia.


Dalili za mapungufu ya potasiamu

  • } Majani huonjesha dalili ya kama kuungua kwenye njia ya jani na kuendelea.

  • } Kwa lugha ya kitaalamu huitwa “chlorosis.”

  • } Mimea inakuwa dhaifu kwa mashambulizi ya magonjwa.

  • } Salfa inahusika kwenye protini ya mmea ,husaidia vimengényo na vitamini vinavyohitajika kwenye kutengeneza ukijani unaosaidia kuakisi mwanga wa jua


.

  • } Sulfur inapatikana kwenye vitu vingi Kama vile gypsum na mbolea kama ammonium sulfate, SSP and TSP.


Matumizi ya mbolea Asilia/Mboji

  • } Mboji ni urutubishaji wa asili ambao hujirudia wenyewe kwa mtindo wa kuoza. Utengenezaji wa  mboji ni njia ya kurudisha rutuba ya asili kwenye udongo kwa njia ya kuozesha vitu.

  • } Matokeo yake ya mwisho ni kutoa mbolea asili ambayo ni rahisi kutengeneza, na ambayo ina virutubisho vingi bila gharama

  • } Mboji huwa ni faida kutokana na uozaji wa asili ambao hutokea kwenye vitu vyote vyenye uhai.

  • } Vitu vyenye uhai ni kama vile majani, miti na mabaki ya vyakula.wakati wa uozaji vitu hivi hugeuka na kuwa rutuba inayorudia kwenye udongo

  • } Udongo hupoteza virutubisho baada ya kutumika sana .

  • } Matumizi ya mbolea za asili nayo ni mazuri katika kuendeleza udongo kwa ajili ya ukulima.

  • } Pia mbolea za asili/mboji husaidia kuzuia mmomonyoko wa ardhi

  • } Inaruhusu mmea kupata rutuba kwa urahisi kutoka kwenye udongo.

  • } Pia hufanya mmea usiwe dhaifu kwahiyo huzuia wadudu waharibifu kushambulia mmea.

  • } Mboji hutoa virutubisho kwa muda mrefu kwasababu ya uendeleaji wa kuoza polepole.

  • } Madini yaliyopo katika mboji husaidia kuyeyusha madini mengine yaliyo kwenye udongo,

  • } Hufanya madini yenye rutuba yapatikane zaidi kwa mimea. Madini hayo huimarisha sehemu laini za mizizi na hivyo kuipa mizizi uimara wa kuweza kupata maji na virutubisho kwa njia ya mizizi


Hitimisho

  • } Mbolea ni kitu muhimu sana katika udongo kwa sababu mazao huitaji virutubisho katika udongo na baada ya udongo kutumika kwa muda mrefu , virutubisho hupotea.

  • } Kuvirudisha virutubisho, mbolea inahitajika inaweza ikawa ya chumvichumvi au ya asili hii hutegemea na udongo uliopo katika sehemu hiyo.

  • } Kila sehemu ina udongo wa aina yake na unahitaji virutubisho vya aina yake kwa wingi au kiwango kidogo.

  • } Kwa hiyo uwekaji wa mbolea katika udongo lazima utumie utaalamu ambao mkulima amepata kutoka kwa wataalamu wa kilimo au uzoefu.

VYAKULA VINAVYOONGOZA KUONGEZA AKILI KWENYE UBONGO


BILA shaka ubongo ni miongoni mwa viungo muhimu vya binadamu lakini ni watu wachache sana wanaoutilia maanani. Ubongo ndiyo kiungo kinachohusika na utendaji kazi wote wa mwili na ndiyo unaowezesha mwili kuishi maisha ya furaha au karaha.
Hata hivyo, wakati mwingine utendaji kazi wa mwili unaweza kuwa siyo mzuri kutokana na sababu mbalimbali zinazoathiri ubongo, mojawapo ikiwa ni kukosekana kwa lishe bora na staili ya maisha inayotakiwa kuimarisha ufanisi wa ubongo.
Chakula ni moja ya sababu za msingi kabisa za kuimarisha ufanisi wa ubongo na kuzuia magonjwa mengine ya akili. Lakini kwa bahati mbaya watu wengi hawajui wale vyakula gani kwa lengo la kujenga akili na kuimarisha ubongo.

Ifuatayo ni orodha ya vyakula ambavyo vinaongoza kwa kuimarisha utendaji kazi mzuri wa ubongo:

MAFUTA YA SAMAKI
Mafuta ya samaki ni muhimu kwa ubongo na mfumo wa fahamu. Ulaji wa samaki wenye minofu kama samoni (salmon) na dagaa, utaweza kupata faida hizo kwa sababu aina hii ya samaki ina kiasi kingi cha mafuta ya Omega 3 ambayo huimarisha utendaji kazi na mawasiliano kati ya ubongo na seli za mwili moja kwa moja.

PILIPILI KALI
Pilipili kali nayo huwa ni chakula kikubwa cha ubongo kwa sababu ina kiwango kingi cha Vitamin C ambayo huhitajika zaidi kwenye ubongo, pilipili inaaminika kuwa na kiwango kingi cha vitamin hiyo kuliko hata machungwa.

MBEGU ZA MABOGA
Mbegu za maboga zina kiwango kingi cha madini ya ‘Zinc’ ambayo husadia kuongeza kumbukumbu (memory). Kuna njia nyingi za kula mbegu za maboga, moja wapo ni kuzikaanga na kula kama karanga, ukila kiasi cha kiganja kimoja kwa siku, inakuwa poa.

NYANYA
Nyanya ni muhimu sana kwa sababu huzuia magonjwa ya ubongo (brain disease) kutokana na kuwa na kirutubisho aina ya ‘Lycopene’ chenye uwezo wa kuzuia magonjwa nyemelezi yanayoweza kutokea. Hivyo ulaji wa nyanya utakusaidia kukupa kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali, yakiwemo ya akili.

BROKOLI
Brokoli ni mboga ya majani aina fulani kama maua ya maboga, ambayo nayo inafaida sana kwenye ubongo, ina vitamin K, C na inatoa kinga ya mwili. Vitamin K inahusika moja kwa moja na utendaji kazi mzuri wa ubongo na husaidia kuzuia magonjwa yatokanayo na uzee.

KARANGA
Aina zote za karanga zina vitamin E, ambayo huzuia tatizo la upotevu wa kumbukumbu na pia zina mafuta yenye afya yanayohitajika mwilini.

MAYAI
Mwisho ni mayai ya kuku, ambayo yana kirutubisho aina ya Choline. Kirutubisho hiki huzalishwa mwilini kwa kiwango kidogo tu, hivyo kwa kula mayai (ya kienyeji) utaweza kuongeza kiwango cha kirutubisho hicho mwilini kwa kiwango kikubwa na hivyo kuimarisha afya ya ubongo.

Ijumaa, 14 Aprili 2017

KILIMO CHA BAMIA


 BAMIA
Asili ya mboga hii ni Afrika ya Kati na ya Mashariki, lakini kwa sasa zao hili limekwisha enea katika sehemu nyingi za kitropiki, kama Visiwa vya Caribbean, Malaysia na Philipines.

Urefu wa mmea huwa kati ya meta moja na mbili. Matunda yake hufikia urefu wa sentimeta 10 hadi 20, na huchumwa kabla hayajakomaa sana na hupikwa pamoja na nyama, samaki au mboga nyingine. Majani yake huchumwa yakiwa bado machanga na kutumiwa kama mboga nyingine za majani.

Aina za bamia zinazojulikana zaidi ni Clemson Spineless, Emerald Green, White Velvet, Perkins Mammoth na Dwarf Prolific.

Ustawishaji: Zao hili hustawi katika mete 1000 kutoka usawa wa bahari na hushindwa kuvumilia hali ya baridi kali. Hustawi katika katika aina nyingi za udongo na huhitaji mvua za wastani. Mimea yake haitumii chakula kingi kutoka ardhini. Iwapo ardhi haina rutuba ya kutosha inapendekezwa kuweka mbolea ya takataka au samadi.

Kupanda: Kwa kawaida mbega za bamia hupandwa moja kwa moja katika bustani, lakini pia kwanza zinaweza kupandwa kwenye kitalu na kuhamishwa baadaye. Mbegu zimiminwe kidogo kidogo na miche ifikiapo urefu wa sentimeta 10 hadi 15, idadi yake ipunguzwe. Umbali wa unaopendekezwa ni sentimeta 40-50 kati ya mimea na sentimeta 70-80 kati ya mistari. Kilo moja hadi moja na nusu ya mbegu hutosha robo hekta ya bustani (zaidi ya nusu eka hivi).

Mbegu za bamia huota kwa shida, mara nyingi huchukua siku nane hadi 12 kutokeza. Ili kurahisisha uotaji, inapendekezwa kwanza kuweka mbegu katika chombo chenye maji ya vuguvugu kwa muda wa saa 24.

Iwapo unyevu wa ardhi hautoshi, inapendekezwa kutumia mojawapo ya njia za kumwagilia maji bustanini. Mimea ifikiapo urefu wa nusu meta hivi wakulima wengine huondo ncha zake kwa kuamini kwamba wingi na ubora wa matunda huongezeka. Bamia huwa tayari kuchumwa baada ya miezi 2 tangu kupandwa na huendelea kwa muda mrefu.

Magonjwa: Mosaic Virus- Huu ni ugonjwa mbaya sana, majani huwa na madoamadoa na huumbuka. Haki hii hupunguza mazao. Nyunyizia dawa za sumu kuua wadudu.

Alhamisi, 13 Aprili 2017

ATHARI ZA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA


MADHARA YA DAWA ZA KULEVYA:
Matumizi na biashara ya dawa za kulevya yameendelea kusababisha madhara makubwa mbalimbali nchini yakiwemo ya kiafya, kijamii, kiuchumi, kimazingira, kisiasa na kiusalama.

KIAFYA:
Dawa za kulevya zimeendelea kuleta madhara makubwa kiafya yakiwemo magonjwa ya akili, utegemezi wa dawa za kulevya, magonjwa ya mapafu, moyo, ini na figo. Aidha, matumizi ya dawa za kulevya yaliendelea kusababisha vifo vya ghafl a hasa miongoni mwa wajidunga kutokana kuzidisha dozi. Pia, matumizi ya dawa hizo yameendelea kuchangia kuenea kwa maambukizi ya VVU, kifua kikuu na virusi vya homa ya ini aina ya B na C. Watumiaji wengi wameendelea kukabiliwa na magonjwa ya meno na ngozi yakiwemo majipu, vidonda na ukurutu. Dawa za kulevya zimeendelea kusababisha kupungua kwa nguvu za kiume, ugumba, utasa na kuzaliwa kwa watoto wenye ulemavu, njiti na wenye matatizo ya ukuaji wa kiakili na kimwili. Jedwali Na.8 linaonesha viwango vya maambukizi ya magonjwa mbalimbali kwa watumiaji waliojitokeza kupata matibabu kwenye hospitali za Muhimbili.

KIUCHUMI:
Matumizi ya dawa za kulevya huongeza mzigo kwa taifa kwa kuwa hupunguza nguvu kazi na husababisha uharibifu wa mali. Vilevile, gharama za udhibiti zikiwemo utoaji wa elimu kwa umma, uteketezaji wa mashamba ya bangi, uendeshaji wa kesi, kuwatunza wafungwa magerezani na kuwatibu watumiaji huongeza mzigo kwa taifa na jamii kwa ujumla.

Biashara ya dawa za kulevya husababisha mfumuko wa bei unaotokana na fedha za biashara hiyo kuingizwa kwenye mfumo halali. Aidha, matumizi ya dawa zakulevya husababisha utoro mashuleni au kazini, kusitisha masomo au kufukuzwa kazi. Kwa ujumla, matumizi na biashara ya dawa za kulevya vimeendelea kuchangia kuongeza umaskini nchini.

KIJAMII:
Dawa za kulevya zimeendelea kusababisha mmomonyoko wa maadili katika jamii. Utumiaji na biashara ya dawa za kulevya mitaani husababisha tabia hiyo kuzoeleka na hivyo kuwavutia watu wengine hasa watoto kujiingiza kwenye tatizo hilo na kuchangia kuharibika kwa kizazi kijacho.Aidha, matumizi ya dawa ya hizo huchangia migogoro ya kifamilia katika jamii jambo linaloweza kuzisambaratisha kabisa. Wazazi ambao hutumia dawa za kulevya, huonesha mfano mbaya kwa watoto wao na jamii kwa ujumla. Pia, kumekuwepo na ajali zilizosababishwa na uendeshaji wa magari na mashine huku waendesha vyombo hivyo wakiwa wametumia dawa za kulevya. Ajali hizo mara kwa mara zimekuwa zikisababisha ulemavu na vifo vingi. Wajidunga hutupa ovyo mabomba ambayo huweza kusababisha majeraha kwa wapita njia au maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

Watumiaji wamekuwa wakijihusisha na tabia na vitendo viovu vikiwemo wizi, uporaji, biashara ya ngono na ubakaji. Jamii imekuwa ikiamini kuwa matumizi ya dawa za kulevya ni jambo la kujitakia, hivyo kuwanyanyapaa na kuwabagua watumiaji. Vitendo na muonekano wao huwafanya wasikubalike katika jamii jambo linalosababisha kuendeleza vitendo vyao vya uhalifu na utumiaji wa dawa za kulevya. Halikadhalika, kosa la kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya huambatana na adhabu kali ikiwemo kifungo cha maisha jambo ambalo linawatenga wahusika na familia zao pamoja na jamii. Biashara ya dawa za kulevya huhusisha rushwa kubwa ambayo huathiri utoaji haki kwa wananchi na utawala bora. Wafanyabishara wa dawa za kulevya hutumia sehemu ya faida wanayopata kusaidia jamii ambayo huwaonea aibu kuwachukulia hatua pindi wanapojihusisha na vitendo viovu.

Wafanyabiashara hujitumbukiza kwenye vitendo vya kihalifu kama utekaji nyara, ugaidi, mauaji ya kikatili, vita vya wenyewe kwa wenyewe na ujambazi, hivyo kusababisha uvunjifu wa amani. Vilevile, wafanyabiashara wa dawa za kulevya huweza kuwarubuni watendaji wa vyombo vya udhibiti wa dawa za kulevya kuvujisha siri hivyo kuhatarisha maisha ya watendaji na raia wema.

KISIASA:
Wafanyabiashara wa dawa za kulevya huweza kuwashawishi wapiga kura kwa kutumia rushwa kuwachagua viongozi watakaosimamia maslahi yao pindi watakapokuwa madarakani. Biashara ya dawa za kulevya huweza kuchochea machafuko ya kisiasa na kuweza kupindua serikali iliyopo madarakani. Halikadhalika, nchi inayojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya huharibu taswira ya nchikimataifa na kusababisha madhara mbalimbali ikiwemo raia wake kutoaminika na kupata usumbufu mkubwa wanapokuwa kwenye nchi nyingine.

KIMAZINGIRA:
Kilimo cha bangi kinachofanyika kwenye vyanzo vya maji na kwenye ardhi oevu husababisha kukauka kwa mito na kuleta ukame. Pia, ukataji miti ovyo na uchomaji moto wa misitu kwa ajili ya kuandaa mashamba ya bangi husababisha mmomonyoko wa udongo.

NB:
Kila ifikapo tarehe 26 mwezi wa 6 kila mwaka,hua ni siku ya kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya duniani.

Jumatano, 12 Aprili 2017

MADHARA YA BANGI


Bangi ni neno ambalo hutumika kuelelezea sehemu iliyokaushwa ya maua, mbegu, mche na majani ya mmea ujulikanao kama Indian hemp. Uko mitaani bangi ina majina mengi na watumiaji wake wameipa majina kama: dope, nyasi, majani, mche, ganja, magugu, kitu, sigara kali, blanti na mboga.

Kwa kitaalam “cannabis” huelezea aina mbali mbali za dawa za kulevya zitokanazo na mmea wa
Indian hemp ambazo ni bangi (marijuana) na hashish.

Aina hizi za dawa zitokanazo na mmea huu ziko katika kundi la dawa za kulevya ziletazo maruweruwe
(hallucinogen) au dawa zinazoathiri ubongo na kubadili jinsi tunavyotazama mambo katika uhalisia wake.Kuna zaidi ya aina 400 za kemikali katika mmea huu na kemikali ya kulaumiwa inayohusika na mabadiliko haya katika ubongo hujulikana kama tetrahydrocannabinol (THC). Kiasi cha THC hutofautiana kulingana na eneo ulikolimwa mmea wa Indian hemp.

Kama tulivyoona bangi ni sehemu iliyokaushwa ya majani, mbegu,maua, na mche na huwa na rangi ya kijani,kijivu au brauni na bangi ni dawa ya kulevya ambayo hutumika kinyume cha sheria katika sehemu nyingi duniani.

Bangi hutumika kwa kuvuta moshi kutoka katika msokoto, sigara iliyoungwa au bomba maalum ya kuvutia moshi wake. Ni mara chache huchanganywa katika chakula, kuliwa kama mboga au kutengeneza kinywaji. Wakati mwingine watumiaji hupukutisha sigara na kujaza bomba la sigara bangi au bangi iliyochanganywa na dawa nyingine za kulevya kama cocaine na aina hii hujulikana na watumiaji kama “blunt”

Mtumiaji anapovuta msokoto wa bangi, huanza kufanya kazi baada ya dakika chache na mvutaji huanza kuhisi mapigo ya moyo yakienda mbio, mapokeo ya uhalisia huanza kubadilika na kuona vitu visivyo katika uhalisia (ndoto za mchana/maruweruwe).Matokeo haya ya muda mfupi baada kuvuta moshi wa bangi, huweza kudumu kwa muda wa saa mbili hadi nne au kuendelea kwa muda mrefu zaidi ikitegemea na kiasi cha THC kilichovutwa na ukali wake.

Mara nyingi wavutaji wa bangi huvuta moshi kwa nguvu ndani ya mapafu na kuushikilia kwa muda mrefu ili kuongeza ufanyaji kazi wa THC ukilinganisha na anayevuta sigara na hii husababisha madhara makubwa katika mapafu ya mvutaji. Mbali na maudhi kama kukohoa na koo kuwasha, imeonekana kuwa uvutaji wa aina hii wa moshi unamweka mvutaji katika hatari mara tano zaidi ya kupata saratani ukilinganisha na mvutaji sigara.

Matatizo ya ubongo yanayopelekea kuathiri afya ya akili ni ugonjwa mbaya uwapatao wavutaji wa bangi. Anayevuta bangi huwa na uwezo mdogo wa kumbukumbu na pia humuondolea uwezo wa asili wa kufanya maamuzi yaliyo sahihi ukilinganisha na mtu asiyevuta bangi.

Jumamosi, 8 Aprili 2017

Vyakula bora kwa afya ya mama na mtoto


Lishe ni muhimu kwa ukuaji wa mtoto – hili si jambo geni sana. Lishe bora ni lazima kwa watoto wadogo sababu wanatakiwa kukua vizuri – kimwili na kiakili.

Je lishe bora ni ipi?

Lishe bora ni chakula chenye virutubisho vyote muhimu kwa kiasi na uwiano sahihi ili kuuwezesha mwili wa mtoto kupata siha nzuri (afya bora). Wataalamu wanachambua zaidi kwa kusema kuwa lishe bora ina virutubisho aina sita, ambayo ni: Wanga, Protein, Mafuta, Vitamin, Madini na Maji.

Je vyakula gani ni bora ?

Lishe bora inatakiwa kuwa na mboga za majani, matunda, protini, wanga na madini ya kutosha. Hizi zinapatikana kwenye vyakula aina tofauti, na kuna vyakula vingine vina virutubisho vingi kwa pamoja.

Mfano wa vyakula vyenye lishe bora kwa kiwango kinachofaa ni kama mboga za majani, mafunda, nafaka asilia, vyakula vya protini (mayai, maharage, nyama n.k) na vyakula vyenye mafuta yasiyohifadhiwa mwilini.
Watoto wanagawanywa kwenye makundi ya aina mbili : Kuzaliwa hadi miezi 6 na kuanzia miezi 6 na kuendelea. Haya makundi ni muhimu sababu watoto waliopo kwenye makundi haya wanatofautiana aina za vyakula wanavyokula. Ni muhimu kuzingatia hili sababu huu ndio muda muhimu zaidi katika ukuaji wa mtoto.

Lishe ya mtoto mchanga hadi miezi 6


Inashauriwa kuwa mtoto mchanga – tangu anazaliwa hadi afikapo miezi 6 – asipewe kitu chochote zaidi ya maziwa ya mama, hii ikiwa inamaanisha hata maji ya kunywa. Maziwa ya mama yana virutubisho vyote muhimu (pamoja na maji) vinavyohitajika kwenye ukuaji mzuri wa mtoto na kumpa kinga ya magonjwa mbalimbali.

Photo by Google

Lishe ya mtoto kuanzia miezi 6


Mtoto akishafika umri wa miezi 6, anaweza kuanza kula vyakula mbali mbali. Inashauriwa mtoto aanze kupewa vyakula mbali mbali kidogo kidogo ili apate kuzoea. Vyakula hivi lazima view vimepondwa, au viwe kwenye mfumo wa uji au maji sababu mtoto anakuwa hana meno yaliyokomaa au wengine wanakuwa hawajaanza kabisa kuota meno.

Lishe ya Mama


Ukizungumzia mtoto hutoweza kuacha kuzungumzia mama. Mama ndiyo chanzo kikubwa cha chakula kwa mtoto tangu anazaliwa hadi anakuwa huru kula chakula cha kawaida. Kwa mwanamke mwenye umri wa kubeba ujauzito au mwenye ujauzito, ni muhimu kula vizuri ili kujenga afya ambayo ndio chanzo kikubwa cha virutubisho kwa mtoto tumboni na baada ya kuzaliwa. Ili kuwa na siha nzuri, vyakula vyote vinatakiwa kuwa na uwiano mzuri wa virutubisho.

Inatakiwa kuzingatiwa kuwa, vyakula vya mtoto viwe vya kuongezea lishe, lakini ni vizuri mtoto akiendelea kunyonya maziwa ya mama hadi atakapofikisha miezi 24. Maziwa ya mama ni muhimu katika kumfanya mtoto akue vizuri, hasa katika miezi 24 ya mwanzo. Inashauriwa kuwa, kama hakuna kikwazo – mfano: ugonjwa wa maambukizi unaoweza kumdhuru mtoto – ni vizuri mama amnyonyeshe mtoto kwa muda mrefu zaidi ya miezi sita (6).

Faida kubwa ya kunyonyesha ni kusaidia ubongo wa mtoto kukua vizuri zaidi sababu maziwa ya mama yanatoa virutubisho kwa wingi kuliko vyakula atakavyokula yeye moja kwa moja. Hii ni kwa sababu, tumbo la mtoot linakuwa halijazoea kusaga vyakula tofauti, hivyo maziwa ni chakula kinacholeta virutubisho vinavyotumika moja kwa moja mwilini.

Umuhimu wa lishe bora


Kama ilivyoelezwa mwanzo, lishe bora ni muhimu. Zifuatazo ni baadhi ya faida apatazo mtoto anayepata lishe bora:

  • Kuimarisha mfumo wa kinga mwilini na kuufanya mwili kupambana kirahisi na magonjwa kama utapiamlo (kwashiorkor) na kiriba tumbo

  • Kujenga siha nzuri (afya bora)

  • Kuleta furaha na Amani

  • Kusaidia ukuaji wa mwili na akili

  • Kuleta nguvu na kusaidia mwili kufanya kazi vizuri


Madhara ya lishe duni


Kama mtoto akiwa na lishe duni, haya yatakuwa madhara yake:

  • Kupata magonjwa mara kwa mara sababu anakosa kinga madhubuti dhidi ya magonjwa

  • Kudumaa kukua mwili na akili

  • Uwezekano mkubwa wa kupata ulemavu sababu mifupa inakuwa laini na haiwezi kustahimili uzito wa mwili.

  • Upungufu wa damu hivyo kudhoofisha afya ya mtoto

  • Kupata utapiamlo (Kwashiorkor)

  • Kupoteza maisha katika umri mdogo

Ijumaa, 7 Aprili 2017

Ufugaji Bora wa Bata Mzinga


Kabla ya kuanza ufugaji wa bata mzinga ni lazima kuhakikisha una chakula cha kutosha kwa sababu ulishaji wa ndege hawa kadri wanavyokua huwa na gharama kubwa zaidi. Ni muhimu pia kujifunza kwa undani na kufahamu namna ya kutunza vifaranga wa bata mzinga kwa kuwa hufa kwa urahisi sana. Pia, unapaswa kujikita kutafuta soko kwa sababu wanapokuwa ni vigumu kuwatunza kwa muda mrefu kutokana na ukubwa wa gharama ya chakula.


Wafugaji wachache kati ya wengi waliojaribu kuwafuga ndege hawa na kufanikiwa hata kufikia malengo yao ni kutokana na kuzingatia lishe kamili. Pamoja na hayo, wapo wafugaji ambao walishindwa kutokana na magonjwa pamoja na gharama ya utunzaji.


Chakula

Chakula cha bata mzinga hakina tofauti na cha kuku. Vifaranga wanahitaji kupata lishe kamili yenye protini kwa wingi ili waweze kukua vizuri. Vifaranga kwa siku za awali wanahitaji kiasi cha asilimia 27 ya protini mpaka wanapofikia umri wa wiki sita. Baada ya hapo mfugaji anaweza kupunguza hadi kufikia asilimia 18, na kuendelea hivyo hadi wanapokomaa. Kutokana na gharama ya kununua chakula kuwa kubwa, unaweza kutumia reseheni ifuatayo kwa ajili ya kutengeneza chakula cha bata mzinga wewe mwenyewe.


Mahitaji



  • Mahindi 5kg (yasiyokuwa na dawa)

  • Karanga 5kg

  • Dagaa 5kg

  • Mashudu 10kg

  • Chokaa 5kg (chokaa inayotumika kwa lishe ya mifugo)


Namna ya kutengeneza chakula
Twanga au saga pamoja kiasi cha kulainika kisha walishe vifaranga. Mchanganyiko huu hutegemeana na wingi wa bata mzinga unaowafuga. Hakikisha kila bata anapata chakula cha kutosha na chenye uwiano ulioelekezwa. Pia waangalie mara kwa mara kuhakikisha wana chakula cha kutosha.


Uhifadhi
Hifadhi chakula cha ziada kwenye mifuko au debe kisha weka sehemu isiyo na unyevu.


Kutaga

Bata mzinga huanza kutaga anapofikisha umri wa mwaka mmoja. Ndege hawa wana uwezo wa kutaga kati ya mayai 15 hadi 20 kwa mara ya kwanza na kisha kuhatamia. Anapoendelea kukua huweza kutaga hadi mayai 30. Hii ni kulingana na lishe nzuri atakayopatiwa.


Kuhatamia

Bata mzinga anaweza kuhatamia mayai 17 hadi 20. Mayai hayo huhatamiwa kwa siku 28 na huanza kuanguliwa vifaranga kwa muda wa siku 3, kuanzia siku ya 28 hadi 31. Baada ya hapo mayai yaliyosalia bila kuanguliwa hutakiwa kutupwa kwa kuwa hayatoanguliwa tena na hayafai kwa matumizi mengine.


Utunzaji wa vifaranga

Baada ya vifaranga kuanguliwa, watenge na mama yao kwa kuwaweka kwenye banda safi lisilopitisha baridi. Unaweza kuwawekea taa ya kandili au ya umeme endapo upo kwenye sehemu unakopatikana.


Banda

Ni vyema banda liwe limesakafiwa au banda la asili la udongo usiotuhamisha maji. Pia, unaweza kutumia banda lenye mbao au mabanzi kwa chini. Unaweza pia kutandaza maranda kwenye mabanda. Hakikisha kuta za banda zimefunikwa vizuri ili kuwakinga dhidi ya baridi. 


Maji

Kama ilivyo ndege wengine, bata mzinga pia wanahitaji kupatiwa maji masafi na ya kutosha wakati wote. Wawekee maji katika chombo ambacho hawatamwaga na wanakifikia vizuri. Hakikisha maji hayamwagiki bandani kwani kwa kufanya hivyo banda litachafuka na kukaribisha magonjwa kwa urahisi. Ni vizuri kuwalisha bata mzinga vyakula vingine kama majani. Majani husaidia kuwapatia protini: mfano; kunde, fiwi na aina nyingine za majani jamii ya mikunde huhitajika zaidi kwa kiasi cha 25% hadi 30%.


Magonjwa

Bata mzinga hushambuliwa na magonjwa kama taifodi, mafua na kuharisha damu. Wanapougua ni rahisi kuambukiza kuku, bata na ndege wengine wanaofugwa kwa haraka sana. Pia, ndege hawa husumbuliwa na viroboto wanaosababishwa na uchafu wa banda hasa linapokuwa na vumbi.


Chanjo

Bata mzinga wanatakiwa kupatiwa chanjo ya ndui (mara moja kila mwaka), kideri (kila baada ya miezi mitatu), gumboro (kwa muda wa wiki tano – ukiwapa jumatatu, basi unawapatia kila jumatatu ya wiki), na vitamini A mara baada ya kuanguliwa.