• TANZAKILIMO TANZANIA

    Pata taarifa sahihi kuhusu kilimo na ufugaji,kwa weledi wa hali ya juu

  • WATAALA WA KILIMO NA UFUGAJI

    Tunakupatia ushauri wa kitaalam katika maswala yote ya kilimo na ufugaji,toka kwa wataalam wetu waliobobea kwenye nyanja nzima ya kilimo. Wasiliana nasi kwa simu namba +255 675 117 151.

  • UNATAFUTA MASOKO YA MAZAO YAKO? UNATAFUTA MAZAO YA KUNUNUA?

    Tanzakilimo inakuunganisha na wakulima/wanunuzi na wadau wote wa maswala ya kilimo. Wasiliana nasi leo tukuunganishe na wadau....

Jumatano, 26 Desemba 2018

KUWA MILIONEA KWA KULIMA TANGAWIZI


Tangawizi ni aina ya zao la kiungo ambalo sehemu inayotumika ni tunguu (rhizome) ambalo huonekana kama mizizi ya mmea. Asili ya zao hili ni maeneo ya kitropiki ya bara la Asia na hasa katika nchi za India na China.


Zao hili linazalishwa kwa wingi kutoka katika nchi ya Jamaica. Hapa nchini zao hili hulimwa katika mikoa ya Kigoma, Tanga, Morogoro, Pwani, Mbeya na Kilimanjaro.

Tangawizi hutumika kama kiungo katika kuongeza ladha, harufu na kuchangamsha katika vinywaji (kama chai, soda, juisi, vilevi n.k) na vyakula mbalimbali kama mikate, biskuti, keki, nyama za kusaga, achari n.k. Hutumika pia katika viwanda vinavyotengeneza madawa ya tiba mbalimbali kama dawa za meno, kikohozi, tumbo na muwasho wa ngozi n.k. pia hutumika katika vipodozi kama poda n.k).


AINA ZA
TANGAWIZI 

Hakuna uthibitisho wa aina za tangawizi ambazo
hulimwa hapa nchini ila kuna dalili ya kuwa na aina za White Africa (Jamaica)
na Cochin (flint); hii huwa na tunguu ngumu zenye nyuzi.

TABIA YA MMEA 
Tangawizi ni mmea unaotambaa chini ya ardhi,
wakati wa masika hutoa majani juu ya ardhi. Jamaica ina rangi hafifu ya kahawia
na tunguu fupi wakati Cochin ina tunguu fupi zaidi lenye ngozi ya rangi iliyo
kati ya kijivu na nyekundu. Mmea una urefu wa futi mbili na majani yake ni
membamba marefu ambayo hufa kila mwaka yakiacha tunguu ardhini likiwa hai. Maua
ya mmea huu yana rangi nyeupe au manjano.

HALI YA HEWA NA
UDONGO 
Zao hili hustawi katika maeneo yenye hali ya
kitropiki, kutoka usawa wa bahari hadi mwinuko wa mita 1,500 au zaidi. Huhitaji
mvua kiasi cha mm.1,200-1,800 na joto la wastani wa nyuzi za sentigredi 20-25.
Hustawi vema katika udongo tifutifu wenye rutuba na usiotuamisha maji.

MMEA WA TANGAWIZI

UPANDAJI 
Zao la tangawizi hupandwa kwa kutumia vipande
vya tunguu vyenye kichipukizi kizuri angalau kimoja na huweza kukatwa katika
urefu wa sm.2.5-5. Wakati mwingine, vichipukizi vinavyopatikana katika kumenya
tangawizi huweza kuhifadhiwa na kutumika kwa kupanda. Kiasi cha kilo 840-1700
cha vipande vya tunguu huweza kutumika kwa kupanda katika hekta moja. Nafasi
inayotumika kupanda ni kati ya sentimita.23-30 kwa 15-23 na kina cha
sentimita.5-10 na mara nyingi hupandwa katika matuta. Baadhi ya mazao huweza
kupandwa katika shamba la tangawizi ili kuweka kivuli chepesi ingawa si lazima
kivuli kiwepo. Inashauriwa kumwagilia maji endapo mvua inakosekana.

Wiki 1-2 kabla ya kupanda weka mbolea ya samadi
au mboji kiasi cha tani 25-30 kwa hekta na kwa kukuzia weka kiasi cha NPK kwa
uwiano wa kilo 36:36:80. Tandaza nyasi shambani kuhifadhi unyevunyevu hasa pale
kivuli kinapokosekana. Palizi hufanywa mara magugu yanapoota, dawa ya kuua
magugu, kama simazine au round up hutumika.

Magonjwa na
wadudu: 
• Madoa ya majani yanayosababishwa na
viini vya magonjwa viitwavyo Colletotrichum zingiberis na Phyllosticta
zingiberi.
• Kuoza kwa tunguu; kunasababishwa na
viini viitwavyo Pithium spp
• Mizizi fundo; inasababishwa na
Meloidegyne spp.

UVUNAJI 

Tangawizi huweza
kuwa tayari kwa kuvuna kati ya miezi 6-10 baada ya kupanda, wakati majani yake
yanapogeuka rangi kuwa njano na mashina kusinyaa. Tangawizi inayohitajika kwa
kuhifadhi kwenye kemikali (preserved ginger in brine) huvunwa kabla haijakomaa
kabisa, wakati ile iliyokomaa kabisa huwa kali zaidi na huwa na nyuzi hivyo
hufaa kwa kukausha na kusaga. Mavuno hutofautiana kulinganana na huduma ya zao,
mavuno yanaweza kuwa kiasi cha tani 20-30 cha tangawizi mbichi huweza
kupatikana.

USINDIKAJI 

Tangawizi
ikisindikwa utapata unga, mafuta maalum (essential oils) n.k. Tangawizi
iliyovunwa huweza kumenywa, kukatwa na kukaushwa juani au mara nyingine
huchovywa katika maji yaliyochemka kwanza na ndipo kukaushwa au hukamuliwa
mafuta. Pia tangawizi husindikwa na kuhifadhiwa kwenye chupa zikiwa
zimechanganywa na sukari na/au chumvi au bila kuweka kitu chochote. Hata hivyo
tangawizi ina Kiasi cha mafuta cha 16.0-18.0%.

GHARAMA ZA
UZALISHAJI NA MAPATO


Gharama ya hekari moja

Kukodi shamba Tshs.=100,000/=

Mbegu 200, 000/=


Kulima 100,000/=

Kupanda 100,000/=

Kupalilia x 4 @ 90,000/= jumla = 360,000/=

Mbolea / samadi 150,000/=

Jumla 1,010,000/=

Mapato kwa hekari.

Ekari moja ya maandishi inatajwa kutoa kilo 8,000 hadi 10,000. Katika hali halisi, kwa uzoefu wangu, ekari moja hutoa kati ya kilo 4000 hadi 6,000. Kutegemeana na kama umeandaa shamba kwa wakati, umefanya palizi kwa wakati, uwepo wa mvua za kutosha na hali ya rutuba ya shamba lako.

Ghalama hizi hutegemea sana na msimu zinaweza shuka au kupanda zaidi.





MASOKO





Sokoni tangawiz huuzwa sh 5000 mpaka 6000 kwa kg soko linapokua zuri, pia kuna msimu hushuka bei mpaka sh 2000 kwa kg.





Kwa masoko ya Tangawizi wasiliana nasi kwa simu namba 0675 117 151, nasi tutakutafutia msoko ya uhakika.



Alhamisi, 6 Desemba 2018

viatamishi (incubators)




Wafugaji wengi wanaonesha kuvutiwa na njia ya utotoleshaji wa mayai unaofanywa na mashine maalumu za kutotolesha mayai maarufu kwa jina la viatamishi (incubators) .Wengi wana kiu ya kutaka kujua gharama, faida, hasara na upatikanaji wa mashine hizi.Kwa kuthamini mchango wa wafuatiliaji wa website hii, nimelazimika kuitumia wiki hii kulielezea hili swala kwa upana wake.

.Viatamishi ni nini?   Hizi ni mashine maalumu zinazotumika kurahisisha utotoleshaji wa mayai ya aina zote  ya kuku wa asili na wale wa kisasa. Pia, inaweza kutumika kwa mayai ya kwale, bata na kanga.Mashine hizi hutofautiana ukubwa, lakini pamoja na tofauti hiyo, bado kila moja ina uwezo wa kutumia muda mfupi kutotolesha mayai, tofauti na muda anaoutumia kuku kuatamia hadi kupata vifaranga.Aina za viatamishiKwa jumla, mashine hizi zote zina kazi moja tu ambayo ni utotoleshaji, japo zimetofautishwa kwa mifumo yake ya kiuendeshaji.Mfumo wa kwanza unazijumuisha mashine zote zinazototolesha mayai kwa kujiendesha zenyewe(automatic).Mfumo wa pili unaziunganisha mashine zote zinazofanya kazi kwa kuendeshwa kwa msaada wa kibinadamu.

Mashine zinazojiendesha zenyewe zinatumika sana kibiashara kwa sababu zinarahisisha kazi tofauti na ilivyo kwa zile zinazoendeshwa na binadamu.Mashine hizi zina faida kubwa kwani si rahisi kuharibu mayai kutokana na kuwa na mashine ndani ambayo kazi yake ni kusaidia kutawanya joto kwenye mayai.Uzuri wake ni kwamba hata joto likizidi uwezekano wa kuharibu mayai haupo kwa sababu feni inasaidia kupunguza joto ndani ya mashine.Kundi la pili linajumuisha mashine zinazofanya kazi zake kwa kutumia uwapo wa mtu muda wote.Aina hii ya mashine hutumia upepo wa kawaida kuendesha zoezi la utotoleshaji, haina feni maalum lakupoza joto.Hii ina maana lazima mtu awe karibu na mashine wakati wote wa utotoleshaji ili aweze kufanikisha mchakato wote.Sifa za viatamishi Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa mashine hizi hazitofautiani sana, ukiachilia mbali ukubwa na mfumo wa uendeshaji. Zipo mashine zenye uwezo wa kutotolesha mayai mengi zaidi kwa pamoja, na nyingine kulingana naudogo wake zinalazimika kutotolesha mayai machache kwa muda mfupi pia.Kwa kawaida mashine nyingi za utotoleshaji hutumia umeme kidogo wa unaokadiriwa kuwa waVoltage:110V- 220V.Ukifanikiwa kupata mashine bora, unajijengea uhakika wa kutotolesha asilimia 95 ya mayai yote.

Unazijuaje mashine bora? Si jambo rahisi kuzijua mashine bora, lakini unaweza kutazama baadhi ya vitu muhimu kama vile tochi maalumu yenye uwezo wa kukagua uhai wa mayai yaliyomo ndani ya mashine.Zipo mashine zenye uwezo wa kila trei ya mayai kuwa na sehemu ya kuangulia vifaranga, kuangalia mfumo maalumu ‘full Automatic’ unaoweza kugeuza mayai, kudhibiti joto na unyevu ndani ya mashine.Jambo muhimu zaidi ni kuhakikisha unatumia mashine yenye uwezo wa kutunza joto kwa muda wasaa sita mara baada ya umeme kukatika.

Viatamishi vya mafuta :Ni muhimu pia kueleza kuwa mbali ya nishati ya umeme, viko vitamishi vinavyoweza kujiendeshakwa kutumia nishati ya mafuta kama ya taa au petrol. Kwa kawaida aina hizi za viatamishi huwa na gharama ndogo.Kwa Watanzania na hata viwanda vidogo vimekuwa vikitengeneza aina hizi za viatamishi. Ni muhimu kutafuta taarifa za viatamishi hivi kutoka kwa wataalamu wa ufugaji au wafugaji wakubwa.



Jumapili, 23 Septemba 2018

UFUGAJI BORA WA SAMAKI


Ufugaji wa samaki unakua kwa kasi sana hapa nchini tanzania kutokana na kuonekana kua na faida sana. hivyo nimeamua leo nikupe elimu kidogo ambayo itakusaidia wewe mfugaji ambaye ungependa kujikita katika ufugaji huo.


SIFA ZA ENEO LA KUFUGIA SAMAKI
Sio kila mahali hufaa kwa ufugaji wa samaki, ila mahali ambapo ni sahihi, zifuatazo ni sifa za eneo bora la kufugia samaki.


  • eneo linalo fikika kwa urahisi

  • eneo tulivu na lenye usalama wa kutosha

  • eneo ambalo linavibali vyote vya umiliki

  • lazima liwe na maji ya kutosha kwa kipindi chote utakacho fuga

  • eneo ambalo halina mmomonyoko wala historia ya mafuriko

  • eneo lenye uwezo wa kutuamisha maji

  • eneo ambalo soko lake sio la shida
    UTENGENEZAJI WA BWAWA
    Kuna aina mbali mbali za kutengeneza mabwawa ya samaki inategemea na eneo, kiasi cha samaki unao taka kufuga, aina ya samaki na hali ya uchumi.aina hizo ni

    • bwawa la kuchimba udongo bila kujengea(earthen pond)







    • bwawa la kuchimba na kujengea 


      



     UPANDIKIZAJI WA VIFARANGA/MBEGU ZA SAMAKI KATIKA BWAWA

    Kabla vifaranga hawaja safirishwa ni vyema kuwatoa katika bwa kubwa wanalo ishi na kuwaweka katika vibwawa vidogo vidogo  kati ya masaa 24 hadi 72 kuendana na umbali wa safari bila kuwapa chakula chochote kile.



    • baada ya kuwasafirisha mfugaji  atakiwi kuviweka kwenye bwawa moja kwa moja ila inatakiwa maji yalio tumika katika kuwasafirisha yabadilishane joto na maji ya bwawa ambalo wataenda kuishi. hivyo mfugaji anatakiwa kuliweka kontena ambalo vifaranga wamo ndani ya bwawa ambalo wataishi kwa dakika 30 hadi 35 bila kuwafungulia, baada ya hapo kontena liina mishwe taratibu ili kuwezesha maji ya bwawa na yaliyo kwenye kontena kubadilishana na baadae vifaranga watatoka taratibu,


    endapo hautafanya hivyo  unaweza kusababisha vifaranga vyote kufa kutokana na mabadiliko   ya joto ambayo yanaweza kutokea ghafla.




    • unatakiwa kusafirisha vifaranga wako mda ambao hali ya hewa inakua sio joto yaan mda wa jion na asubuhi ili kuwezesha vifaranga kuimili misukosuko ya safari na bila kupatwa na joto kali.


    CHAKULA NA UTUNZAJI WA SAMAKI BWAWANI

    • Samaki hutakiwa kupewa chakula angalau mara 2 kila  siku  unatakiwa kuzingatia mda sahihi wa kuwapa chakula yaan asubuhi saa 3-4 na jion saa 9 -10 samaki upewa vyakula tofauti kulingana na aina
      tabia ya ulaji wa samaki ni kama ifuatavyo 



      1. samaki wanao kula nyama (sangara, kambale)

      2. samaki wanao kula mimea carps

      3. samaki wanao kula mchanganyiko (perege,sato na samaki wa maji ya chumvi mfano kibua)


      zingatia kuweka maji  ambayo ni safi 



      TARATIBU ZA ULISHAJI WA SAMAKI


      UMRI(wiki)                          UZITO(gm)             KIASI CHA CHAKULA KWA SIKU (gm)

      1-2                                           5-10                                   1

      2-3                                           20-50                                 2

      3-5                                           50-110                              3

      5-7                                            110-200                           4

      7 nakuendelea                          200 na zaidi                     5



Ijumaa, 7 Septemba 2018

FAIDA NA HASARA ZA KUTUMIA KILIMO CHA GREEN HOUSE


GREEN House, kwa tafsiri isiyo rasmi, ni nyumba kitalu. Nyumba ambayo imejengwa kukidhi mahitaji ya mimea. Nyumba hizi hujengwa kwa ustadi mkubwa wa kitaalumu kwa kuzingatia baadhi ya mambo muhimu.

Baadhi ya mambo hayo muhimu ni pamoja na hali ya hewa ya eneo husika joto, baridi, mwanga wa jua, uelekeo wa upepo, muinuko kutoka usawa wa bahari, aina ya udongo, ubora wa maji, mteremko wa eneo husika.

Lakini pia kuna mambo ya kuzingatia kama aina za malighafi za kutumika na ubora wake nailoni, neti kivuli, mbao au chuma, plastiki, upatikanaji wa maji, kufikika kwa eneo, muinuko wa jengo (Gutter height), ni muhimu kuzingatia urefu kutoka usawa wa ardhi kabla ya kuezeka green house

Mazao yanayooteshwa kwenye mfumo huu yako ya aina maalumu kwa maana ya aina ya mbegu za kutumika/hybrid/F1, zenye sifa mbalimbali kama urefu, ipo namna yake ya uwekaji mbolea, kumwagilia ambazo ni njia tofauti sana na inavyofanyika katika mashamba ya wazi.

Sababu za watu kupenda kutumia aina hii ya kilimo

Kwanza kabisa sababu kubwa inayowasukuma wengi kuingia katika kilimo hiki ni ile ya kutoa mavuno mengi katika eneo dogo, kwa mfano kuna taarifa ambazo huenezwa na watu kuwa unaweza kupata tani 60 za zao kama nyanya ndani ya green house kwa eneo la upana wa mita 8 na urefu wa mita 15.

Aina hii ya taarifa ni moja ya kichocheo ambacho huwavutia sana watu, kwani mtu hupiga haraka hesabu za mapato na kuona kuwa inalipa.

Pia taarifa nyingine ambazo huwatia watu faraja na matumaini juu ya kilimo hiki ni kwamba ni aina ya mfumo ambao hauna usumbufu badala yake mtu hujipatia fedha zake kwa haraka.

Ukiacha taarifa za namna hiyo pia zipo zile zinazosema kuwa ukimaliza kujenga tu jengo la Green House, basi wewe ni tajiri yaani utakuwa na kazi ya kupanda na kusubiri kuvuna tu hata kwa miaka 10 mfulululizo.

Kwa taarifa kama hizi hufanya mtu kuwaza mapato makubwa, kuwa ikiwa kwa labda miezi 3 tu nina tani 60 za nyanya kwa eneo la mraba la mita 120, na anaambiwa unavuna tu, na jengo ni imara linadumu kwa miaka 10 bila matengenezo wala marekebisho.

Pamoja na kwamba aina hii ya kilimo imekuwa na faida lakini pia imekuwa na changamoto zake zinazowakumba wakulima wanaotumia mfumo huu wa kilimo.

Kwa maeneo ya miji mikubwa kama, Dar es Salaam na mikoa mingine zipo baadhi ya green house ambazo zimejengwa mwaka jana, lakini wamiliki wake wamezitelekeza na wengine wamezibomoa baada ya kuona wanapata mashambulizi ya magonjwa na wadudu.

Wapo baadhi ya wakulima kwa kupata taarifa zisizo sahihi waliaminishwa kuwa hakuna magonjwa wala wadudu wanaoshambulia mazao yaliyopo ndani ya green house, hivyo wakulima wakaishi kwa kujiamini kwa kujua kuwa wanachosubiria ni mapato ya tani 60.

Matokeo yake wamejikuta wanapata magonjwa na wadudu kama mazao ya shamba wazi, unakuta ni green house ya nyanya lakini ndani unakuta kuna changamoto ya wadudu.

Kuna baadhi ya wakulima mazao yao yamenyauka na kufa yakiwa ndani ya green house, kuna wakulima walijenga green house kwa matumaini ya kupata pesa ya haraka na wameishia kupata hasara kwa kuwa hawakupata ushauri sahihi na mazao yao yamekauka pia kama vile yapo kwenye shamba la wazi.

Mara nyingi green house hizi zimekuwa kwenye eneo lenye joto kubwa ikilinganishwa kuwa kimo chake kinapaswa kuwa chini ya mita 2.5, hivyo kufanya joto kuwa kali sana na mazao kunyauka, ambapo wataalamu wanashauri kuwa ni bora zaidi kujengwa kulingana na mazingira ya eneo au mkoa husika.

Mavuno kidogo.

Wapo wakulima waliolima ndani ya green house, mbali ya kwamba walikuwa wakiaminishwa kuwa watapata mavuno mengi yatakayowafanya kurudisha gharama zao ndani ya msimu mmoja matokeo yake imekuwa kinyume kabisa (mavuno hafifu na yasiyo bora) jambo ambalo linatokana na kutozingatia kanuni bora za uandaaji wa aina hii ya kilimo.

Kukosekana kwa soko

Baadhi ya wakulima waliowekeza kwenye kilimo hiki wamekuwa wakiaminishwa kuwa kwa kuwa ni mavuno ya green house, basi yatapata soko zuri muda wowote atakaovuna, jambo ambalo ni kinyume ambapo kwa sababu hizo wamekuwa wakizalisha mazao bila ya kuwa na hofu ya kukosa soko.

Na hivyo kujikuta kwamba pindi inapofikia wakati wa mavuno imekuwa kilio kwani mazao hayo yamekuwa yakipata bei sawa tu na yale ya mashamba ya kawaida huku wakati mwingine mazao hayo yakiharibika kabisa kwa kukosa soko.

Ubora hafifu wa mazao

Kwa mujibu wa wataalamu wanabainisha kuwa mazao huwa si mazuri na kutofanana hatua zote za ukuaji.

Kwani baadhi ya wakulima waliaminishwa kuwa mazao yote yaliyomo ndani ya green house yatakuwa katika kiwango sawa na yatafanana kwa kuwa yapo katika mazingira mazuri ya aina moja.

Hivyo kumfanya mmiliki kuamini kuwa kwa kuwa ni green house ni lazima ukuaji uwe bora na mzuri, hata kama hatofanya jitihada zozote, yeye atasubiri kuvuna na kupata pesa tu.

Ili kuweza kufanikiwa kwenye kilimo hiki cha green house basi kuna mambo ya kuzingatia kabla ya kuingia katika aina hii ya kilimo.

Wataalamu wa kilimo hiki wanasema kuwa kwanza kabisa ili mtu aweze kufanikiwa basi hana budi kuhakikisha kuwa anaweka juhudi, umakini na malengo katika jambo husika, kwani unaweza kuwa na green house lakini bado ukaambulia hasara na usifaidike na chochote kinyume na matarajio yako.

Na hivyo kwa sababu hiyo ukajikuta uko sawa tu kama siyo nyuma ya yule aliyelima kilimo cha kawaida ambacho ni cha wazi.

Lakini pia jambo jingine la kuzingatia ni kuhakikisha kuwa unafahamu vizuri kilimo hiki, ikiwamo pia kutambua mbegu zilizobora na zinazoendana na soko unalolilenga kwani kinyume na hivyo unaweza kujikuta unaambulia hasara.

Hivyo ni busara kabla ya kuanza aina hii ya kilimo ni vizuri iwapo utatafuta ushauri kwa watu waliokwisha kufanikiwa kupitia mfumo huu lakini pia kutafuta taarifa mbalimbali juu ya aina hii ya kilimo.

Hii itakusaidia kujua changamoto na namna gani unavyoweza kuzikabili ikiwamo, gharama, magonjwa kwani usipokuwa makini unaweza kujikuta unakabiliana na changamoto zilizoko kwenye kilimo cha kawaida cha shamba wazi ilihali una green house.

Pia jambo jingine la kuzingatia ni kuhakikisha kuwa unafanya utafiti wa kina kabla ya kuamua kuingia kwenye aina hii ya kilimo, hii itakusaidia kuweza kulibaini soko linavyokwenda na upande na kuvuna wakati gani.

Pia hakikisha kuwa unapata fundi ambaye ni mzoefu kwenye uandaaji huu wa green house ikiwamo kujiridhisha kwanza kuhusu ubora wa kazi zake alizowahi kufanya kabla ya kuingia makubaliano ya kukutengenezea green haouse yako.

Jumatatu, 13 Agosti 2018

HIZI NDIZO SABABU ZA KUKU WAKO KUDONOA MAYAI NA KUDONOANA


Kati ya mambo ambayo mfugaji anatakiwa kuwa nayo makini ni pamoja na tabia za kila siku za mifugo yake. Kuna wakati kuku wanakuwa na tabia za kudonoa na kula mayai,pia kudonoana wenyewe kwa wenyewe. Tabia hii si nzuri na si ya kawaida. Hizi hapa chini ni sababu zinazopelekea kuku kuwa na tabia hizi:

SABABU ZA KUKU KULA MAYAI.

1. Ukoo- Hapa utakuta ndo ukoo/uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai,

2. Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai,chakula kikiiwa kichache hawashibi hupeleka kutafuta njia mbadala ya kushiba. 

3. Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, na jua kwamba kwenye yai kuku huwa anatafuta lile ganda la juu pekee sema anapo donoa na kulipasua yai hujikuta anakula na ute na kiini ila yeye lengo lake hasa ni ganda la juu.

 4. Kuku kutagia sehemu nyeupe sana yenye mwanga mkali upelekea kuku kula mayai,kuku anapenda kutagia sehemu fichifichi yenye mwanga hafifu kidogo ndo anakua huru zaidi kutaga.

5. Mayai kukaa muda mrefu bila kukusanywa baada ya kutaga- Hapa ni kwamba mayai yanapo kaa muda bila kukusanywa na kama yapo sehemu ya wazi ni rahisi wao kudonoa.

6. Lishe mbaya-kuku akipata lishe mbaya ya chakula humpelekea kudonoa chakula,kuku anapaswa kupata chakula chenye virutubisho vyote.

7. Nafasi ndogo-kuku wanapaswa kupata nafasi kubwa yakupumzika na kulia chakula.

8. Vyombo vichache-bandani unapaswa kuwa na vyombo vya chakula na maji vya vyakutosha kuondoa kusukumana na kutokula kwa raha.

9. Kukosa shughuli yakufanya-kuku wakila wakishiba unapaswa kuwafungia majani km kabeji ili wawe bize mda wote.

NAMNA YA KUZUIA KUKU KUDONOANA AU KULA MAYAI 

1. Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba.

 2. Mayai yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani. 

3. Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai alilo taga.

4. Madini joto ni muhimu sana. 

5. Kuku wenye tabia za kula mayai unaweza chinja au kuuza. 

6. Kuweka idadi ya kuku inayolingana na sehem ulionayo.

 7. Usizidishe mwanga. 

8. Banda liwe safi.

9. Weka vyombo vya kutosha. 

10. Wape lishe bora

11. Wape kuku shughuli kwa kuwawekea bembea na sehemu ya uwazi kwa ajili ya mazoezi. 

12. Kata midomo ya juu.

13.Epuka ukoo wenye tabia hizo.

Kwa leo naishia hapa,nakutakia mafanikio mema kwenye ujasiriamali wako, Mungu awabariki sana.
⁠⁠⁠