Jumatatu, 20 Machi 2017

KILIMO CHA MATANGO

ni zao linalopendelea hali ya hewa ya joto na husitawi vema kati ya nyuzi joto 18°C hadi 35°C

Udongo Hustawi vizuri katika udongo tifutifu wenye rutuba usiotuamisha maji

Maandalizi ya shamba Lima shamba kwa trekta, kwa ng’ombe ama kwa jembe la mkono kwa kina cha sentimita 30 hadi 45


Weka matuta ya mwinuko yenye upana wa mita 1 hadi 1.5 kutoka kati ya tuta na tuta

Upandaji Zipo aina mbili za upandaji,
1.ya kwanza ni ile ya kupanda mbegu moja kwa moja na

2. ya pili ni ile ya kupanda mbegu katika trei na kuhamisha baada ya siku 8 hadi 10.

Njia ya kupanda mbegu moja kwa moja ni rahisi lakini ile ya kupanda katika trei ni bora zaidi kwani shamba hujaa vizuri katika nafasi na hukua haraka na kuzaa mavuno mengi

Pima mashimo ya kupandia katika umbali wa sentimita 20 hadi 25 kutoka shina hadi shina mstari mmoja kwa tuta na sentimita 40 katika mfumo wa zig-zag pande zote mbili za tuta na kupanda

Mbolea kianzio iwekwe katika kila shimo na kupanda endapo miche kutoka katika trei itatumika Hakikisha shamba lina unyevu wa kutosha kabla ya kupanda



Palizi Palilia shamba mara kwa mara ili kuhakikisha shamba halina magugu Magugu hudhibitiwa kwa palizi ya jembe, kung’oa kwa mkono ama matumizi ya viuagugu.



Njia nyingine ni matumizi ya plastiki maalum kuzuia magugu yaani ‘plastic mulch’

Mbolea Tumia mbolea ya DAP wakati wa kupanda na kisha tumia NPK yenye uwiano mmoja kama, 18:18:18, 17:17:17 ama 16:16:16 baada ya wiki tatu toka Usegekaji
Tumia nguzo za unene wa inchi 2 na kamba ili kuinua mimea na matunda yasiguse ardhi na kuoza

Uchavushaji
Hii ni muhimu sana kuzingatiwa kwani tango huchavushwa kwa wadudu na si upepo
.Bila wadudu kama nyuki uzalishaji huathrika sana.

Ni muhimu kupanda mazao kama alizeti na maua mbali mbali yanayopendwa na wadudu wachavushaji ili kuhakikisha uwepo wa wadudu hao shambani.

Aidha inapo-lazimu ni vema kuweka mizinga kadhaa ya nyuki katika shamba la tango

Mavuno  huanza baada ya siku 40 hadi 45 kutegemea na aina pamoja na hali ya hewa

Related Posts:

  • kilimo cha ngano na faida zake kilimo cha ngano na faida zakeUtangulizi:Hapa nchini, zao la ngano linalimwa zaidi katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, na Manyara, kwa upande wa kaskazini na Iringa, Mbeya na Rukwa kwa upande wa kusini. Ngano ni zao la… Read More
  • KILIMO BORA CHA VITUNGUUKITUNGUU-ONION (Allium cepa)Vitunguu ni zao la pili ambalo hutumika karibu kila siku katika mlowa familia za kitanzania. Vitunguu vina chukua nafasi kubwa katikamatumizi ya mboga hasa kwa wakazi wa mijini. Vitunguu hutumikaka… Read More
  • KILIMO CHA BAMIA BAMIAAsili ya mboga hii ni Afrika ya Kati na ya Mashariki, lakini kwa sasa zao hili limekwisha enea katika sehemu nyingi za kitropiki, kama Visiwa vya Caribbean, Malaysia na Philipines.Urefu wa mmea huwa kati ya meta mo… Read More
  • KILIMO CHA MATANGOni zao linalopendelea hali ya hewa ya joto na husitawi vema kati ya nyuzi joto 18°C hadi 35°CUdongo Hustawi vizuri katika udongo tifutifu wenye rutuba usiotuamisha majiMaandalizi ya shamba Lima shamba kwa trekta, kwa ng’ombe … Read More
  • KUWA MILIONEA KWA KULIMA TANGAWIZITangawizi ni aina ya zao la kiungo ambalo sehemu inayotumika ni tunguu (rhizome) ambalo huonekana kama mizizi ya mmea. Asili ya zao hili ni maeneo ya kitropiki ya bara la Asia na hasa katika nchi za India na China. Zao hili … Read More

0 comments:

Chapisha Maoni